Connect with us

News

Kesi ya Mihadarati ya bilioni 8.2 kusikizwa Mahakama ya Mombasa

Published

on

Kesi ya usafirishaji wa dawa za kulevya zenye thamani ya shilingi bilioni 8.2 iliendelea kusikilizwa katika mahakama ya Shanzu, shahidi wa pili ambaye ni afisa wa Jeshi la Wanamaji nchini akielezea mahakama kuwa jahazi lililokamatwa likiwa na dawa hizo halikuwa na utaifa wowote.

Akitoa ushahidi mbele ya Mahakama, Meja Mohamed Abdulrahman alisema chombo hicho kilikuwa kikifuatiliwa kwa muda mrefu na idara za kijasusi kutokana na tuhuma za usafirishaji wa mihadarati katika eneo la Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika.

Kwa mujibu wa ushahidi, jahazi hilo lililojulikana kama MV Igor lilikamatwa umbali wa maili 350 kutoka pwani ya Mombasa likiwa halina bendera wala nyaraka zozote za usafirishaji.

Mahakama pia ilielezwa kwamba meli hiyo ilihusishwa na tukio la kushusha mzigo unaoshukiwa kuwa wa dawa za kulevya katika mji wa Maputo nchini Msumbiji mnamo Juni mwaka 2025.

Katika operesheni hiyo, maafisa wa wanamaji walikamata watu sita wanaodaiwa kuwa raia wa Iran na kupata bidhaa nyeupe inayoshukiwa kuwa dawa za kulevya ikiwa imehifadhiwa kwenye makasha madogo.

Vifaa vingine vilivyopatikana ni pamoja simu tano za rununu, simu ya setilaiti, kadi za utambulisho zenye maandishi ya Kiarabu pamoja na kadi za benki na laini kadhaa za simu.

Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa huku Mahakama ikitarajiwa kutembelea makao makuu ya Jeshi la Wanamaji kushuhudia vielelezo vilivyokamatwa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending