News

Mikakati ya kudhibiti migogoro ya mipaka yaidhinishwa Kwale

Published

on

Gavana wa kaunti ya Kwale, Fatuma Achani ametangaza kujengwa kwa jengo jipya la ofisi za utawala wa kaunti hiyo katika wadi ya Mackinnon gatuzi dogo la Samburu, ili kulinda na kukabiliana na migogoro ya mipaka baina ya kaunti ya Kwale na Taita Taveta.

Akizungumza katika makao makuu ya kaunti hiyo mjini Kwale, Gavana Achani alisema ofisi hiyo pia itasaidia kupunguza kero kwa wakaazi wa eneo hilo kutafuta huduma mbalimbali za serikali ya Kwale.

Gavana Achani pia alisema serikali ya kaunti ya Kwale inaendeleza mikakati katika kuhakikisha kuna miradi ya maendeleo ambayo inatekelezwa kwa manufaa ya wakaazi.

‘’Kulikuwa na vita baina ya Kwale kaunti na Taita Taveta tuliposhinda katika kesi ile tukaonelea ili kulinda kabisa mikapa yetu tujenge ofisi pale Makina’’ alisema Achani.

Vilevile, gavana Achani alizungumzia suala la kugatuliwa kwa huduma mbalimbali za kaunti hiyo hadi mashinani kupitia ujenzi wa ofisi za utawala katika wadi zote 20 za kaunti hiyo ili kupeleka huduma za serikali karibu na wananchi.

‘’Tunalenga kupunguzia mwananchi huduma badala ya kuzifuata kwa kaunti anaweza kuzipata mashinani’’ aliongeza Achani

Haya yanajiri baada ya serikali ya kaunti ya Kwale kushinda kesi ya mzozo wa mipaka uliokuwepo katika eneo la Macknon kati ya kaunti ya Kwale na Taita Taveta mwezi Julai, 2024.

Taarifa ya Janet Mumbi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version