News

Murkomen: Serikali Kubuni Kitenga Maalum Kuchunguza Mizozo ya Ardhi Pwani

Published

on

ARDHI-

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen amesema serikali inalenga kubuni kitenga maalum cha maafisa wa usalama watakaochunguza mizozo ya ardhi katika eneo la Pwani.

Katika kikao na Wanahabari, Waziri Murkomen amesema hatua hiyo itahakikisha ardhi zote zenye mizozo zinatatuliwa kwa usawa kwani idadi kubwa ya wakaazi wa Pwani wamekuwa wakihangaishwa katika ardhi zao.

Murkomen amesema Wizara ya usalama kwa ushirikiano na ile ya ardhi nchini na jamii mashinani watahakikisha utata huo unapata suluhu la kudumu sawa na kuwawezesha wananchi kupata hati miliki za ardhi zao.

Wakati huo huo amedokeza kwamba analenga kubuni sera maalum itakayosaidia kuajiri maafisa wa usalama kila mwaka ili kuimarisha usalama wa taifa huku akiwaonya wakenya dhidi ya kushiriki ufisadi wakati wa zoezi la kusajili makurutu.

Waziri Murkomen yuko katika ukanda wa Pwani kwa ziara ya wiki moja kutathmani maswala ya kiusalama ambapo alianza na kaunti ya Mombasa kisha kaunti ya Kwale, Kilifi, Lamu, Tanariver na kaunti ya Taita taveta kabla ya kukamilisha ziara hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version