Sports
Mwanariadha Kipyegon Kutimka Chini Ya Dakika 4,Paris
Bingwa wa Olimpiki wa dunia mbio za mitaa 1500 Mkenya Faith Kipyegon atakua anaingia kwenye daftari za kumbukumbu kwa kuwa mwanamke wa kwanza kukimbia mile moja chini ya dakika nne mjini Paris Ufaransa.
Mkimbiaji huyo nguli na bingwa mara tatu wa Olimpiki ndiye mshilikizi wa rekodi bora zaidi ya mbio za mitaa 1500 na anatarajiwa kurejea katika mji wa Stade Charlety leo usiku kufanya vile.
Zaidi ya wanaume 200 wamekimbia mile moja kwa dakika nne mwanamke pekee ambaye amekaribia hapo ni Kipyegon ambaye alivunja rekodi yake mwenyewe wa mita 1500 mjini Monaco kwa muda bora wa dakika 4:07.64 mwaka 2023.
Mtimkaji huyo hata hivyo atakua anasaidiwa na vifaa maalum kwenye viatu katika shindano hilo la Break4 kama ilivyokua kwa nguli wa mbio za masafa marefu Eliud Kipchoge alipokimbia chini ya 2 mjini Vienna.
Iwapo atavunja rekodi hiyo atapokea shilingi milioni 13 pesa za kenya.