Sports
Ni Afueni kwa Vilabu vya Ligi kuu baada ya Shirikisho la Soka Kenya (FKF) kutangaza Ongezo la Shilingi Milioni 15
Katika kile kinachoonekana kama msukumo mkubwa kwa Ligi Kuu ya Kenya (KPL), Shirikisho la Soka Kenya (FKF) limetangaza ongezeko kubwa la zawadi ya fedha kwa mabingwa wa ligi, mara tatu yaani kutoka Shilingi milioni 5 hadi Shilingi milioni 15.
Kwa miaka mingi, mabingwa wa ligi wamekuwa wakijipatia zawadi ya kiasi cha kawaida cha Shilingi milioni 5. Hali hiyo inabadilika msimu huu baada ya rais wa FKF, Hussein Mohamed, kufichua Jumanne kwamba shirikisho hilo kwa kushirikiana na wadau wao wa michezo ya kubashiri wameongeza Shilingi milioni 20 kwenye mfuko wa zawadi.
Chini ya mfumo mpya:
-
Mabingwa watapata Shilingi milioni 15,
-
Nafasi ya pili Shilingi milioni 3,
-
Nafasi ya tatu Shilingi milioni 2.
Shirikisho litachangia Shilingi milioni 10 katika mfuko huo, huku kiwango sawa kikitolewa na mdhamini mkuu wa ligi. ✅