Sports
Ni Afueni kwa Vilabu vya Ligi kuu baada ya Shirikisho la Soka Kenya (FKF) kutangaza Ongezo la Shilingi Milioni 15
Katika kile kinachoonekana kama msukumo mkubwa kwa Ligi Kuu ya Kenya (KPL), Shirikisho la Soka Kenya (FKF) limetangaza ongezeko kubwa la zawadi ya fedha kwa mabingwa wa ligi, mara tatu yaani kutoka Shilingi milioni 5 hadi Shilingi milioni 15.
Kwa miaka mingi, mabingwa wa ligi wamekuwa wakijipatia zawadi ya kiasi cha kawaida cha Shilingi milioni 5. Hali hiyo inabadilika msimu huu baada ya rais wa FKF, Hussein Mohamed, kufichua Jumanne kwamba shirikisho hilo kwa kushirikiana na wadau wao wa michezo ya kubashiri wameongeza Shilingi milioni 20 kwenye mfuko wa zawadi.
Chini ya mfumo mpya:
-
Mabingwa watapata Shilingi milioni 15,
-
Nafasi ya pili Shilingi milioni 3,
-
Nafasi ya tatu Shilingi milioni 2.
Shirikisho litachangia Shilingi milioni 10 katika mfuko huo, huku kiwango sawa kikitolewa na mdhamini mkuu wa ligi. ✅
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

