Sports

Simba SC yaikwatua Gor Mahia mechi ya kirafiki Uwanjani Benjamin Mkapa

Published

on

Miamba wa soka nchini Tanzania klabu ya Simba waliwashinda mabingwa wa zamani wa ligi kuu nchini Kenya, Gor Mahia, mabao 2-0 katika mechi ya kirafiki iliyopigwa Jumatano jioni katika uwanja wa kitaifa wa Benjamin Mkapa.

Mchuano huo ulikuwa wa maadhimisho ya siku ya Simba Dei ambapo ni siku ya utambulisho wa wachezaji wapya kilabuni humo.

Wekundu wa Msimbazi Simba walijipatia magoli yao kupitia kwa beki Abdulrazak Hamza na mshambulizi wa raia wa Uganda Steven Dese Mukwala katika kila kipindi.

Timu zote zilitumia mechi hiyo kama maandalizi ya mwisho kabla ya kungoa nanga kwa msimu mpya wa Ligi Kuu ya Kenya na ile ya Tanzania Bara.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version