Sports
Starlets Watambaa Dhidi Ya Crested Cranes Ya Uganda
Timu ya Taifa ya soka akina dada Harambee Starlets imeendeleza ilipoachia mechi ya pili taji la CECAFA ukanda wa Afrika Mashariki baada ya kunyuka Crested Cranes ya Uganda kipigo cha magoli 4-0 mechi ya pili Ugani Azam Sports Complex mjini Dar es salaam Tanzania.
Kiungo wa kilabu ya Kenya Police Bullets Diana Wacera aliwaweka uongozini vipusa wa nyumbani kunako dakika ya 19,Huku nyae beki wa kimataifa Dorcas Shikhobe akiweka kambani goli la pili kunako dakika ya 27,mshambulizi wa kimataifa Violet Wanyonyi Nanjala akifunga goli la tatu dakika ya 29 naye kiungo wa kilabu ya Vihiga Queens Martha Amunyolet akifunga goli la nne na la mwisho dakika ya 81 kipindi cha pili.
Huu ukiwa ni ushindi wa pili kwa timu hiyo chini ya kocha Beldine Odemba katika mechi ya kwanza walishinda Burundi magoli 3-0 siku ya Jumapili.
Katika mechi nyingine Twiga Stars ya tanzania walirindima Burundi magoli 6-0 katika uga uo huo.Kituo kinachofuata kwa Starlets ni dhidi ya Sudan Kusini Alhamisi.