Business

Wahudumu wa Tuktuk walalamikia kupanda kwa bei ya mafuta

Published

on

Wahudumu wa sekta ya uchukuzi wa Tuktuk katika wadi ya Mariakani eneo la bunge la Kaloleni kaunti ya Kilifi wanaendelea kulalamikia gharama ya juu ya bei ya mafuta ya petroli hali ambayo imeathiri biashara zao.

Kulingana na baadhi ya wahudumu hao, bidhaa zisizo na msingi zimeshuka bei ilhali  bei ya mafuta ikionekana kuendelea kupanda jambo ambalo walisema imekuwa changamoyo wa wahubumu wengi.

Wakizungumza na Coco Fm , wahudumu hao wa Tuktuk walidai kwamba tangu kuongezwa kwa bei ya mafuta ya Petroli kwa shilingi nane wengi wao wamepata changamoto hata zaidi huku wakipoteza wateja baada ya kujaribu kuongeza nauli kwa wateja wao.

Hata hivyo, waliitaka serikali kuu  kuingilia  kati swala hilo mara moja kwani asilimia kubwa ya wahudumu hao wanaendelea kupata hasara.

Wakati huo huo  walipendakaza bidhaa ambazo sio muhimu kama vile sigara na Pombe kuongezwa bei na na kupunguza bei za mafuta na  vyakula.

Taarifa ya Pauline Mwango

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version