Business
Wahudumu wa Tuktuk walalamikia kupanda kwa bei ya mafuta
Wahudumu wa sekta ya uchukuzi wa Tuktuk katika wadi ya Mariakani eneo la bunge la Kaloleni kaunti ya Kilifi wanaendelea kulalamikia gharama ya juu ya bei ya mafuta ya petroli hali ambayo imeathiri biashara zao.
Kulingana na baadhi ya wahudumu hao, bidhaa zisizo na msingi zimeshuka bei ilhali bei ya mafuta ikionekana kuendelea kupanda jambo ambalo walisema imekuwa changamoyo wa wahubumu wengi.
Wakizungumza na Coco Fm , wahudumu hao wa Tuktuk walidai kwamba tangu kuongezwa kwa bei ya mafuta ya Petroli kwa shilingi nane wengi wao wamepata changamoto hata zaidi huku wakipoteza wateja baada ya kujaribu kuongeza nauli kwa wateja wao.
Hata hivyo, waliitaka serikali kuu kuingilia kati swala hilo mara moja kwani asilimia kubwa ya wahudumu hao wanaendelea kupata hasara.
Wakati huo huo walipendakaza bidhaa ambazo sio muhimu kama vile sigara na Pombe kuongezwa bei na na kupunguza bei za mafuta na vyakula.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
KPA yaimarisha usafirishaji wa makasha na kampeni za kimataifa
Halmashauri ya bandari nchini (KPA), imeimarisha ushirikiano wake na kampuni ya kimataifa ya usafirishaji kwa njia ya bahari, Maersk, katika juhudi za kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa usafirishaji wa mizigo katika eneo la Afrika Mashariki.
Makubaliano hayo yameafikiwa katika mkutano uliofanyika katika makao makuu ya KPA jijini Mombasa ambapo Mkurugenzi wa Maersk Kanda ya Afrika Mashariki, Tito Okuku, alieleza kuwa kampuni hiyo ina nia ya kupanua shughuli zake zaidi nchini na katika eneo la Afrika Mashariki kwa ujumla.
Moja ya maeneo yatakayopata kipaumbele ni kuimarisha matumizi ya Kituo cha Makontena cha ndani cha Naivasha kinachotazamwa kama kitovu muhimu katika kushughulikia usafirishaji wa mazao ya kilimo kutoka Kenya kwenda masoko ya kimataifa, huku kikitoa njia ya haraka na ya kuaminika kwa wauzaji kufikia masoko ya kimataifa.
Mkurugenzi Mkuu wa KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kukubaliana na hatua hiyo akisema ni wakati mwafaka kwa pande zote mbili kuimarisha ushirikiano huo.
Aidha alibainisha kuwa Bandari ya Mombasa pamoja na vituo vyake vya ndani vinaendelea kushuhudia ongezeko la shehena, na akahakikishia kuwa KPA iko tayari kushughulikia mahitaji yanayoongezeka kupitia maboresho ya miundombinu na huduma.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
Business
Wakulima wa Mananasi Magarini walilia soko
Wakulima wa matunda aina ya nanasi katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi wanaitaka serikali kuwatafutia soko ili kuuza bidhaa zao ambazo zinaendelea kuharibika msimu huu.
Kulingana na wakulima hao hakuna soko ambapo wanaweza kuuza bidhaa hizo kwa bei nzuri hali inayofanya wakulima wengi kuuza kwa bei ya chini ili kuepuka kuharibika kwa katunda hayo.
Wakizunumza na cocofm wakulima hao walisema kuwa kwa sasa wanakadiria hasara kwani matunda ni mengi.
Wakati huo huo wakulima hao wameitaka serikali ya kaunti kujenga viwanda.
Ni kauli ambayo imeongwa mkono na wafanyibiashara wa matunda mjini Kilifi kaunti ya Kilifi ambao walisema kuwa matunda mengi msimu huu huharibika kutokana na idadi ndogo ya wateja.
“Serikali itutafutie soko pamoja na kujenga viwanda ili kusaidia wakulima na wafanyibiashara wa matunda aina ya mamanasi, kuuza matunda yao ili kuawaepushia hasara hasa wakati huu ambapo matunda ni mengi.”
Taarifa ya Pauline Mwango

