News

Wataalam wa uchumi samawati wakataa matumizi ya “Ring Net”

Published

on

Wataalam wa maswala ya uchimi wa bahari nchini wamesistiza marufuku ya uvuvi wa kutumia nyavu aina ya Ring Net wakisema nyavu hizo zinaharibu zao la samaki baharini.

Wakiongozwa na Stanley Chai, wataalam hao walisema nyavu hizo zinafaa kutumika kuanzia umbali wa maili tano baharini kutoka ufuoni hali ambayo wavuvi wa kawaida hapa nchini kwa sasa hawana uwezo wa kufika umbali huo.

Chai alidokeza kuwa nyavu hizo zinapotumika hunasa mayai ya samaki baharini hali inayosambaratisha na kuharibu kizazi cha viumbe hai baharini.

“Watu wetu hawa wavuvi wadogo wadogo wanatumia ndoana, uvuvi wa ring net nitakwambia si uvuvi mzuri hasa kama utakuja kwa maji yasiyo ya kina kirefu, ring net inabeba mpaka mayai ya samaki, ukiona nakala ya sheria zetu ambazo hazijachapishwa kwenye gazeti rasmi la serikali tumesema uvuvi wa ring net uruhusiwe umbali wa maili tano kuendelea na sio chini ya hapo kwa sababu chini ya hapo ndio samaki huzaana”, alisema Chai

Wakati huo huo Chai alisistiza umuhimu wa utekelezaji mpango wa kuingiza samaki nchini kutoka mataifa ya nje ili kuongeza kipato kupitia kodi na kuwezesha wavuvi kwa vifaa bora vya kuendeleza shughuli zao baharini.

“Wale samaki wakubwa tukiwaingiza hapa nchini tusiliseni ile ya dola elfu hamsini, hiyo ni kitu kidogo, yule samaki akiingizwa hapa nchini tunakusanya mabilioni, sasa hizi mabilioni tumesema nini kwa zile nakala ya sheria? tumesema zile pesa zitakazopatikana kwa biashara ya samaki asilimia 70 ziende kwa serikali kuu, asilimia 20 ziende kwa kaunti zinazopakana na bahari hindi, hii asilimia 10 iekezwe kuboresha wavuvi wadogowadogo halafu asilimia 10 ziende kwa vikundi vya maendeleo baharini-BMU, wale wavuvi moja kwa moja wanaweza kununua maboti makubwa nakupata uwezo wa kwenda kule chini”, aliongeza mtaalam Chai.

Kwa mda wavuvi eneo la pwani wamekuwa wakilalamikia serikali kuwafadhili na vifaa vya kisasa vya uvuvi ikiwepo boti zinazostahamili mawimbi baharini ili waweze kufika maji makuu na kuongeza pato la samaki.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version