Sports
William Saliba asaini mkataba mpya na Arsenal kwa miaka mitano ijayo
Beki wa taifa la Ufaransa William Saliba amesaini mkataba mpya wa miaka mitano na kilabu yake ya Arsenal na kusitisha uvumi wa kuondoka Emirate hivi karibuni.
Haya yanajiri Baada ya makubaliano ya maneno wiki iliyopita, beki huyo wa Kifaransa sasa ameweka kalamu karatasi na kujifunga kwa mradi wa muda mrefu wa Arsenal.
Saliba, ambaye alikuwa akivutiwa na vilabu vikubwa ikiwemo Real Madrid kwa mwaka 2026, ameamua kujitolea mustakabali wake Emirates.
Ni taarifa nzuri kwa Arsenal wanaona hii kama hatua muhimu ya kuimarisha safu ya ulinzi kwa muda mrefu kwani beki huyo amekua nguzo muhimu katika kikosi hicho chini ya kocha Mikel Arteta ambao pia wamesajili mabeki wawili Christian Mosquera na Piero Hincapie,