Sports
Kocha Wa Ureno Jose Mourinho Apigwa Kalamu na Fernabache Ya Uturuki
Mkufunzi wa Ureno Jose Mourinho ametimuliwa na klabu ya Fenerbahce ya Ligi Kuu ya Uturuki baada ya michezo sita pekee tangu kuanza kwa msimu mpya.
Sababu kuu ya hatua hiyo ilikuwa ni kichapo dhidi ya Benfica Jumatano usiku, kilichosababisha Fenerbahce kukosa kufuzu kwa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa.
Taarifa kwenye akaunti rasmi ya Fenerbahce katika X ilisomeka: “Timu yetu ya Soka ya Kitaaluma imeachana na Jose Mourinho, ambaye amekuwa kocha mkuu tangu msimu wa 2024-2025. Tunamshukuru kwa juhudi zake kwa timu yetu hadi sasa na tunamtakia mafanikio katika taaluma yake ya baadaye.”
Mourinho, mwenye umri wa miaka 62, aliteuliwa kuwa meneja wa Fenerbahce mwezi Mei 2024, akitia saini mkataba wa miaka miwili. Hata hivyo, kipigo cha 1-0 katika uwanja wa Estadio da Luz kimefupisha muda wake nchini Uturuki.
Kwa mujibu wa jarida la michezo la Uturuki, Spor Arena, uhusiano wa Mourinho na bodi ya Fenerbahce ulikuwa na misukosuko wakati wa dirisha la usajili la kiangazi, huku kocha huyo wa zamani wa Manchester United akikosoa mkakati wa klabu hiyo.
Kocha huyo amewahi kuvinoa pia vilabu vya Chelsea,Manchester United,Spurs,Real na As Roma.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

