Sports
Alexander Trent Arnold Sasa Ni Mali Ya Madrid
Kilabu ya Real Madrid imtangaza kupata sahihi ya beki wa taifa la Uingereza na kilabu ya Liverpool Alexander Trent Arnold.
Miamba hao wa Uhispania inaaminika imelipa kima cha Euro milioni 10 kupata sahihi ya beki huyo ambaye amechezea Liverpool tangu utotoni akitokea kwenye academia ya kilabu hiyo.
Trent mwenye umri wa miaka 26 ametia wino mkataba wa miaka sita kilabuni humo inayomueka hadi mwaka 2031.
Makubaliano hayo yakiwa pia kwamba kilabu ya Madrid italipa mshahara wake wa miezi za June na Julai.
Mchezaji huyo anatarajiwa kuvalia jezi la Los Blancos kwa mara ya kwanza katika fainali ya kombe la Dunia baina ya vilabu mwezi ujao Juni 14.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

