Sports
Bailey Ajiunga Rasmi na As Roma ya Italia Akitoka Aston Villa
Mshambulizi wa Aston villa Leon Bailey amekamilisha uhamisho wa mkopo kutoka Villa Park kwenda klabu ya Roma ya Italia.
Winga huyo wa Jamaica amejiunga na kikosi hicho cha Italia kwa msimu wa 2025-26, huku mkataba huo ukiwa na kipengele cha kununua.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 alihamia Villa mwaka 2021 akitokea klabu ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani kwa dau la pauni milioni 25 na kufunga jumla ya magoli 22 katika mechi 144.
Bailey alifunga magoli 14 msimu wa 2023-24 katika mashindano yote, kiwango bora zaidi katika taaluma yake, lakini msimu uliopita alifunga mara mbili pekee katika michezo 38.
Alisaini mkataba mpya na Villa mnamo Februari 2024 ambao unatarajiwa kumweka klabuni hadi mwaka 2027.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

