Sports
Beldine Odemba Angali Kocha Wa Starlets.
Mkufunzi wa Harambee Starlets Beldine Odemba atarejea kunoa tena kikosi hicho kwenye kinyanganyiro cha Cecafa ukanda wa Afrika Mashariki nchini Tanzania.
Haya yanajiri saa chache tu baada ya mwalimu huyo kubatilisha uwamuzi wake wa awali wa kujiuzulu wadhifa wake kwa kukosa ungwaji mkono kwenye majukumu yake ndaani ya vipusa hao.
Hata hivyo inaaminika baada ya kikao na Rais wa FKF Hussein Mohammed mwafaka imepatikana na sasa kocha huyo anasalia usukani kuiongoza Starlets kombe la cecafa taji ambalo linaanza mwishoni mwa jumaa.
Kocha huyo ambaye ni bingwa na kilabu ya Kenya Bullets alitangaza kujiuzulu baada ya kichapo cha magoli 5-1 mikononi mwa Morocco mechi ya kirafiki.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

