Sports
Bingwa Wa Olimpiki Noah Lyles Kuanza Msimu Monaco
Bingwa wa Olimpiki mbio za mitaa 100 Noah Lyles wa Marekani kuanza rasmi msimu wake mjini Monaco Ufaransa katika msururu wa Diamond Ligi hii leo.
Mtimkaji huyo amekua na jeraha akiwa nje na sasa anarejea ulingoni akitarajiwa kuanza kutetea ubingwa wake katika mbio za mitaa 200 akitarajiwa kumenyana na bingwa wa Olimpiki mbio hizo Letsile Tebogo raia wa Botswana.
Lyles ndiye anashikilia rekodi bora katika mbio hizo baada ya kukimbia muda wa sekunde 19.46 mwezi wa April mwaka 2020 ila hajashiriki katika mashindano yoyote huu msimu.
Tebogo alirejea kwa kishindo wikendi iliopita na kushinda mbio za mitaa 200 mjini Eugene Oregon Marekani kwa muda wake bora wa sekunde 19.76 licha ya kuwa na msimu mbovu hadi sasa na amesema kwamba lengo lake ni kufanya kweli mjini Monaco Ufaransa.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

