Connect with us

Sports

Bingwa wa taifa wa mbio za mitaa 10,000 Gladys Kwamboka angaa mashindano ya Betika Bingwa Fest katika chuo cha walimu cha Shanzu

Published

on

Bingwa wa taifa wa mbio za mita 10,000, Gladys Kwamboka, aling’ara katika mashindano ya Betika BingwaFest kanda ya Pwani yaliyofanyika katika Chuo cha Ualimu cha Shanzu, baada ya kutwaa mataji 2 ya mita 10,000 na 5,000 kwa wanawake.

Kwamboka, mwenye umri wa miaka 29, alishinda mbio za mita 10,000 kwa kutumia muda wa dakika 33:39.5 katika mashindano ya kiufundi, akiongeza kasi katika mita za mwisho na kumaliza mbele ya Brenda Jepchumba Kenei (33:34.0) na Kadogo Jematian (33:44.16).

Baadaye alirejea uwanjani na kutwaa pia taji la mita 5,000 kwa muda wa 16:07.2, akimshinda kwa tofauti ndogo ya sekunde 0.4 Celestine Biwott katika moja ya fainali zilizokuwa na ushindani mkali zaidi siku hiyo. Kadogo Jematian alikamilisha orodha ya washindi kwa kushika nafasi ya tatu kwa muda wa 16:10.5.

Akizungumza baada ya ushindi wake, Kwamboka, ambaye pia ni bingwa wa Afrika wa mwaka 2024, alisema:
“Nimekuwa nikijiandaa ili nipate nafasi ya kushiriki, lakini sikupata fursa mapema msimu huu kwa sababu ya majukumu ya kikazi. Sikutarajia kushinda leo kwa sababu bado najijenga kwa ajili ya msimu, lakini naamini nimefanya vyema.”

Kwa ushindi huo wa mataji mawili, Kwamboka alijinyakulia jumla ya Sh550,000 — Sh300,000 kwa ushindi wa mita 10,000 na Sh250,000 kwa mita 5,000.

Katika mbio za mita 10,000 kwa wanaume, Stephen Muthini alishinda kwa muda wa 29:14.7, akiwashinda Edica Kipkorir (29:28.4) na Joseph Ndirangu (29:30.1) waliomaliza katika nafasi ya pili na ya tatu mtawalia.

Mbio za mita 5,000 kwa wanaume zilishuhudia ushindani mkali huku Abel Kirui akishinda kwa muda wa 13:14.0, akimshinda kwa karibu Victor Kimutai aliyekimbia kwa 13:14.8. Weldon Langat alimaliza wa tatu kwa 13:45.0.

Katika mita 1,500 kwa wanawake, Naomi Korir alionyesha utulivu na kushinda kwa muda wa 4:24.9, akifuatiwa na Celestine Biwott (4:26.5) na Christine Komen (4:27.9). Kwa upande wa wanaume, Kyumbe Munguti alishinda kwa 3:46.8, huku Wilson Larry Merin na Constantine Cheruiyot wakimaliza kwa 3:48.3 na 3:48.4 mtawalia.

Kutoka Tanzania, Winfrida Makenji alitawala mbio za mita 100 kwa wanawake kwa muda wa sekunde 12.3, akiwashinda Maximilla Imali (12.4) na Moureen Wafula (12.5).

Bingwa huyo wa mara nne wa taifa la Tanzania katika mita 100 alisema alifurahia changamoto ya kushindana na wanariadha wapya katika mazingira mapya.

“Hii ni jukwaa zuri sana kwangu,” alisema baada ya ushindi wake.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Sports

Bingwa wa dunia mbio za mitaa 1500 Faith Kipyegon ateuliwa kuwania tuzo za kila mwaka za ‘Laureus World Sportswoman of the Year.’

Published

on

By

Nyota wa mbio za masafa ya kati kutoka Kenya, Faith Kipyegon, amepata uteuzi wake wa tatu mfululizo kuwania tuzo ya Mwanamichezo Bora wa Kike wa Mwaka katika hafla maarufu ya Laureus World Sports Awards, hatua inayozidi kuthibitisha ubabe wake katika kizazi hiki cha wanariadha.

Tuzo hizo, zinazotambuliwa kimataifa kama “Oscars za Michezo”, huandaliwa na Laureus Sport for Good Foundation na hulenga kutambua mafanikio ya kipekee, uthabiti na mchango chanya wa michezo duniani.

Uteuzi wa Kipyegon kwa miaka mitatu mfululizo unaonyesha si tu kipaji chake, bali pia uimara wa kiwango chake cha juu kwa muda mrefu. Mwaka 2024 aliteuliwa baada ya msimu wa kihistoria wa 2023 ambapo alivunja rekodi tatu za dunia na kushinda dhahabu mbili katika Mashindano ya Dunia.

Mwaka 2025 alirejea tena kwenye orodha ya wateule kufuatia mafanikio makubwa katika Michezo ya Olimpiki ya Paris, ambako aliweka historia kwa kuwa mwanamke wa kwanza kushinda medali tatu za dhahabu mfululizo katika mbio za mita 1,500.

Sasa mwaka 2026, anawania tuzo hiyo tena baada ya kuvunja rekodi yake mwenyewe ya dunia ya mita 1,500 na kutwaa taji lake la nne la dunia katika msimu bora wa 2025.

Katika kinyang’anyiro cha mwaka huu, Kipyegon anakutana na ushindani mkali kutoka kwa nyota wengine wa kimataifa akiwemo Sydney McLaughlin-Levrone, Melissa Jefferson-Wooden, Aitana Bonmati, Aryna Sabalenka, na Katie Ledecky.

Uteuzi huu unaendeleza hadhi ya Kipyegon kama mmoja wa wanariadha bora zaidi duniani na fahari kubwa kwa Kenya katika jukwaa la kimataifa.

Continue Reading

Trending