News
Serikali imefanikiwa kutekeleza asilimia 55 ya mageuzi ya polisi
Katibu katika Wizara ya usalama wa ndani Raymond Omollo amesema serikali imefanikiwa kutekeleza asilimia 55 ya mageuzi yanayoendelea ya kitaifa katika idara ya polisi nchini.
Omollo alisema kufuatia mkutano wa ngazi ya juu na kamati ya uongozi ya usalama wa kitaifa ulioongozwa na rais William Ruto iliafikia kutekelezwa kwa mageuzi hayo kwenye idara ya polisi nchini.
Omollo alidokeza kwamba mchakato huo unalenga kuimarisha taasisi za kiusalama, kuboresha utoaji wa huduma na kuboresha mifumo ya polisi nchini.
“Tuko asilimia 55 ya mageuzi yanayoendelea ya kitaifa katika idara ya polisi nchini na kwamba juhudi hizo zitachangia kuimarisha idara ya polisi nchini sawa na kuhakikisha maafisa wa polisi wanapata mazingira bora na salama ya kufanya kazi”, alisema Omollo.
Omollo alisema kumekuwa na maendeleo ya kuridhisha katika maeneo muhimu, ikiwemo mageuzi ya kiutawala, kisheria na ustawi wa ndani ya huduma ya polisi na kwamba mabadiliko ya kimuundo na kiutendaji yanaendelea kutekelezwa.
Aidha, alisema serikali imeanza kutekeleza mareboresho ya mishahara ya polisi, huku awamu ya pili ya marekebisho ya mishahara ikitarajiwa ndani ya miezi miwili ijayo kabla ya utekelezaji kamili.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

