Sports
Bruno Akataa Al-Hilal
Ni taarifa nzuri kwa mashabiki wa kilabu ya Manchester United kwani ,Kiungo na nahodha wa kilabu ya Manchester united Bruno Fernandes amekataa ofa ya pauni milioni 200 kutoka kilabu ya Al-Hilal ya saudia.
Mabingwa hao walikua wametoa ofa hiyo na ada ya ununuzi ya pauni milioni 100 kwa kilabu ya United kupata sahihi ya mchezaji huyo ila inaaminika familia imekua sababu kuu ya Mreno huyo kudinda kuondoka england.
Timu hiyo ilikua imempa kiungo huyo makataa ya wiki moja kuamua iwapo atajiunga nao au la. Hata hivyo baada ya kuketi mezani na mawakala wake na kilabu ya Manchester United inaaminika kwamba mchezaji amekubali kusalia barani Ulaya.
Kilabu ya Al-Hilal ilikua tayari kumpa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 mkataba wa miaka mitatu na mshahara mnono kujiunga nao msimu ujao ila uwamuzi huo umepokelewa vyema na usimamizi wa United ambao hawakua tayari kumwachilia nyota huyo.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

