Sports
Bunge La Taifa Limetambua Team Kenya kwa mafanikio yake katika Mashindano ya Dunia ya Riadha Mjini Tokyo mwaka 2025
Bunge la Taifa limeitambua rasmi nafasi ya kipekee ya Kenya katika Mashindano ya Dunia ya Riadha yaliyokamilika Tokyo, ambapo Timu ya Kenya ilidhihirisha ubabe wake duniani kwa kuvuna idadi kubwa ya medali.
Katika taarifa kwa bunge Jumanne, Spika Moses Wetang’ula aliwapongeza wanariadha kwa kuonyesha ustahimilivu, kipaji na uzalendo wa hali ya juu, akisema kuwa mafanikio yao si tu kwamba yameinua hadhi ya Kenya katika riadha za dunia, bali pia yameamsha tena fahari ya kitaifa.
Kenya ilinyakua jumla ya medali 11: dhahabu 7, fedha 2, na shaba 2, ikimaliza nafasi ya pili duniani na ya kwanza barani Afrika.
Dhahabu: Lilian Odira (800m), Emmanuel Wanyonyi (800m), Faith Kipyegon (1500m), Faith Cherotich (3000m kuruka viunzi na maji), Beatrice Chebet (5000m & 10,000m), na Peres Jepchirchir (marathon).
Spika alisisitiza ushindi wa kihistoria wa Odira na Wanyonyi, walioweka rekodi mpya za mashindano kwenye mbio zao za 800m.
Aidha, aliwapongeza wanariadha wanawake wa Kenya kwa kutwaa medali za dhahabu katika mbio zote za wanawake – hatua ya kwanza kabisa katika historia ya mashindano haya.
“Kenya imekuwa nchi ya kwanza kutwaa dhahabu katika kila mbio ya wanawake kwenye Mashindano ya Dunia. Hili ni jambo la kihistoria linalothibitisha nafasi yetu kama nguvu ya riadha duniani,” alisema Wetang’ula.
Fedha: Faith Kipyegon (5000m), Dorcas Ewoi (1500m).
Shaba: Edmund Serem (3000m kuruka viunzi na maji), Reynold Cheruiyot (1500m).
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

