Connect with us

Sports

Bunge La Taifa Limetambua Team Kenya kwa mafanikio yake katika Mashindano ya Dunia ya Riadha Mjini Tokyo mwaka 2025

Published

on

Bunge la Taifa limeitambua rasmi nafasi ya kipekee ya Kenya katika Mashindano ya Dunia ya Riadha yaliyokamilika Tokyo, ambapo Timu ya Kenya ilidhihirisha ubabe wake duniani kwa kuvuna idadi kubwa ya medali.

Katika taarifa kwa bunge Jumanne, Spika Moses Wetang’ula aliwapongeza wanariadha kwa kuonyesha ustahimilivu, kipaji na uzalendo wa hali ya juu, akisema kuwa mafanikio yao si tu kwamba yameinua hadhi ya Kenya katika riadha za dunia, bali pia yameamsha tena fahari ya kitaifa.

Kenya ilinyakua jumla ya medali 11: dhahabu 7, fedha 2, na shaba 2, ikimaliza nafasi ya pili duniani na ya kwanza barani Afrika.

Dhahabu: Lilian Odira (800m), Emmanuel Wanyonyi (800m), Faith Kipyegon (1500m), Faith Cherotich (3000m kuruka viunzi na maji), Beatrice Chebet (5000m & 10,000m), na Peres Jepchirchir (marathon).

Spika alisisitiza ushindi wa kihistoria wa Odira na Wanyonyi, walioweka rekodi mpya za mashindano kwenye mbio zao za 800m.

Aidha, aliwapongeza wanariadha wanawake wa Kenya kwa kutwaa medali za dhahabu katika mbio zote za wanawake – hatua ya kwanza kabisa katika historia ya mashindano haya.

“Kenya imekuwa nchi ya kwanza kutwaa dhahabu katika kila mbio ya wanawake kwenye Mashindano ya Dunia. Hili ni jambo la kihistoria linalothibitisha nafasi yetu kama nguvu ya riadha duniani,” alisema Wetang’ula.

Fedha: Faith Kipyegon (5000m), Dorcas Ewoi (1500m).
Shaba: Edmund Serem (3000m kuruka viunzi na maji), Reynold Cheruiyot (1500m).

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending