Connect with us

Sports

Carlos Alcaraz asonga raundi ya tatu US Open kwa ushindi wa kasi, Djokovic aponea chupuchupu

Published

on

Mchezaji wa Tenisi Carlos Alcaraz raia wa Uhispania alitinga raundi ya tatu ya US Open hapo jana baada ya kushinda kwa seti tatu mfululizo kwa kishindo, huku Novak Djokovic akitoka nyuma kufanikisha ushindi baada ya kuonyeshwa kivumbi mapema.

Alcaraz, ambaye anaweza kukutana na Djokovic katika nusu-fainali endapo upangaji wa mechi hizo  utafuatwa huko Flushing Meadows, alimfagia Muitaliano Mattia Bellucci 6-1, 6-0, 6-3 katika muda wa saa moja na dakika 36 pekee kwenye uwanja mkuu wa Arthur Ashe Stadium.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22, akiwa mchezaji namba mbili kwa ubora duniani, alitoa mikwaju ya kushambulia 32 katika mchezo wa kutawala dhidi ya Bellucci anayeridhiwa nafasi ya 65 duniani, ambaye mafanikio yake makubwa zaidi katika Grand Slam yalikuwa kufika raundi ya tatu Wimbledon mapema mwaka huu.
“Kwa kweli nimecheza vizuri sana, kuanzia mwanzo hadi mpira wa mwisho,” alisema Alcaraz, ambaye sasa atakutana na Muitaliano mwingine, Luciano Darderi (mbegu ya 32) katika raundi inayofuata.
“Kadri ninavyotumia muda mchache uwanjani ndivyo ilivyo bora zaidi kwangu, nipate kulala mapema,” aliongeza.

Wakati huohuo Jumatano, gwiji kutoka Serbia, Novak Djokovic, alihifadhi ndoto yake ya kunyakua taji la kihistoria la Grand Slam la 25 baada ya kumbwaga Mmarekani aliyeingia kwa kufuzu, Zachary Svajda, kwa seti nne.

Djokovic, hata hivyo, alilazimika kupambana baada ya kupoteza seti ya kwanza kabla ya kutwaa ushindi wa 6-7 (5/7), 6-3, 6-3, 6-1.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 38 alisema ingawa hayupo katika kiwango chake cha juu kwa sasa, anatumai kupata mwendelezo bora kadri mashindano yanavyoendelea.
“Ndio ninachotarajia, kadri ninavyosonga mbele kwenye mashindano ndivyo ninavyohisi vizuri zaidi kuhusu mchezo wangu,” alisema.

Ushindi huo unamweka Djokovic katika raundi ya tatu ya US Open kwa mara ya 19, akilingana na rekodi ya kihistoria, ambapo atakutana na Muingereza Cameron Norrie, aliyembwaga M-Argentina Francisco Comesana 7-6 (7/5), 6-3, 6-7 (0/7), 7-6 (7/4).

Katika mechi nyingine za wanaume Jumatano, Mnorwe Casper Ruud (mbegu ya 12) na finalisti wa US Open 2022, aliondoshwa na Mbelgiji Raphael Collignon baada ya kupoteza 6-4, 3-6, 3-6, 6-4, 7-5.

Mchezaji wa Marekani Taylor Fritz (mbegu ya 4) aliendelea salama kwa kumbwaga M-South Africa Lloyd Harris 4-6, 7-6 (7/3), 6-2, 6-4, huku rodha ya Marekani ikiimarishwa na Frances Tiafoe (mbegu ya 17), aliyemshinda mchezaji wa kufuzu Martin Damm kwa seti nne, 6-4, 7-5, 6-7 (8/10), 7-5.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending