Sports
Chelsea Mabingwa Kilabu Bingwa Duniani
Miamba wa Uingereza kilabu ya Chelsea ndiyo mabingwa wa Fainali ya Kombe la Dunia baina ya vilabu baada ya kutia darasi kabila ya kukalifisha PSG kibano cha magoli 3-0 ugani Metlife jana usiku.
Kiungo mshambulizi Cole Palmer alikua nyota wa mchezo akianza safari ya kuwapa raha mashabiki wa The Blues dakika ya 22 kabila ya kuongeza la pili dakika ya 30 kisha Joao Pedro akifunga la tatu dakika ya 43.
Kilabu ya PSG ilimaliza mechi hiyo wachezaji 10 uwanjani baada ya kiungo wa Ureno Joao Neves kulisha kadi nyekundu dakika za jioni kipindi cha Pili.
Kwa mujibu wa kocha wa Chelsea Enzo Maresca walistahili ushindi kwani walikua timu bora uwanjani huku wakilimbisha sakafu timu yenye uwezo mkubwa Psg.
“Kuanzia Mwanzo tulikua timu bora,iliounda nafasi nyingi ,timu iliyo na kiu ya ushindi tulishinda wenzetu kila sehemu uwanjani.”
The Blues sasa watakua wanapumzika kabila kuanza kuwazia ligi kuu Uingereza mwezi ujao.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

