Sports
Cherotich Amshinda Tena Yavi Mbio Za Oslo.
Riadha
Mkenya Faith Cherotich kwa mara nyingine tena ameweza kumshindabingwa wa Olimpiki mbio za mitaa 3000 kuruka maji na viunzi Winfried Yavi raia wa Bahrain kwa kutumia muda wake bora wa dakika 9:02.60 huku bingwa huyo wa olimpiki akimaliza nafasi ya pili kwa na dakika 9;02;76 naye Marwa Bouzayani wa Tunisia kwa muda dakika 9:06.84.
Hii ni mara ya pili kwa chipukizi huyo kubwaga Yavi ambaye makao yake ni Kenya japo anakimbilia taifa hilo la Bahrain baada ya kufanya hivyo tena msururu wa Doha Qatar mwezi jana.
Katika mbio za mitaa 800 mkenya Emmanuel Wanyonyi aliandikisha muda wake bora wa dakika 1;42.78 na kumaliza wa kwanza mbele ya Mohammed Attaoui wa Uhispania na Djamel Sedjati wa Aljeria waliotumia muda za 1;42.90 na 1;43.96 na kumaliza wa pili na tatu mtawalia.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

