Sports
City Yasajili Wachezaji Watatu
Kilabu ya Manchester City imetangaza kukamilisha uhamisho wa wachezaji watatu tayari kwa msimu mpya baada ya kukamilisha vipimo vya kimatibabu.
Wachezaji hao watatu ni pamoja na beki Rayan Ait -Nouri kutoka kilabu ya Wolves kwa pauni milioni 31 mchezaji huyo tayari amepasi vipimo vya kimatibabu na kumwaga wino mkataba wa miaka mitano na The Citizens.
Wachezaji wengine ni Tijjani Reinders ambaye amejiunga na kilabu hiyo kwa pauni milioni 55 akitokea kilabu ya AC Milan ya Italia kwa mkataba wa miaka mitano pia.
Timu hiyo pia imekamilisha usajili wa winga wa taifa la Ufaransa na kilabu ya Lyon ya Ufaransa Rayan Cherki ambaye anajiunga na kilabu hiyo kwa pauni milioni 45 na ametia wino mkataba wa miaka mitano.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

