Connect with us

Sports

Djokovic akutana na Alcaraz kwenye nusu fainali ya US Open, Sabalenka apenya bila kucheza

Published

on

Mchezaji wa Tenisi Novak Djokovic amefuzu kwenye mechi ya nusu fainali ya US Open dhidi ya Carlos Alcaraz siku ya Jumanne huku bingwa mtetezi wa upande wa wanawake Aryna Sabalenka akitinga nusu fainali bila hata kunyanyua raketi yake.

Djokovic alizima matumaini ya Taylor Fritz ya kuwa Mmarekani wa kwanza kushinda taji la Grand Slam la wanaume tangu mwaka 2003 baada ya ushindi wa seti 6-3, 7-5, 3-6, 6-4 kwenye robo fainali iliyochezwa uwanjani Arthur Ashe Stadium.

Ushindi huo ulimpeleka Mserbia huyo mwenye umri wa miaka 38 ambaye anawinda taji la kihistoria la Grand Slam la 25  kwenye nusu fainali ya kusisimua dhidi ya Alcaraz, anayeshikilia nafasi ya pili duniani kutoka Uhispania, siku ya Ijumaa.

Djokovic alihitimisha ushindi wake pale Fritz, aliyeshika nafasi ya nne kwa ubora, alipofanya kosa la mara mbili la “double fault” kwenye “match point” katika mchezo wa 10 wa seti ya mwisho, na hakuficha furaha yake baada ya kuibuka mshindi.

“Katika mechi ya aina hii, pointi chache tu upande mmoja au mwingine ndizo huamua mshindi,” alisema. “Ilikuwa mechi ya karibu sana. Kwa kweli ingeweza kwenda kwa yeyote.”

Fritz aliachwa akijuta kushindwa kutumia fursa zilizojitokeza, baada ya kufanikisha ushindi wa pointi mbili pekee kati ya 13 katika pambano lililochukua saa tatu na dakika 24.

Mmarekani huyo alipoteza nafasi tano za “break point” katika seti ya kwanza ambazo zingemfanya aongoze 5-4, badala yake akamruhusu Djokovic kuponyoka na kuongoza kwa seti moja.

Baada ya kupambana na kufanikiwa kumsawazisha Djokovic kwa 5-5 katika seti ya pili, Fritz alivunjwa tena mara moja na kupoteza mwelekeo. Djokovic alishikilia na kuchukua uongozi wa seti mbili, na ingawa Fritz alirudi na kushinda seti ya tatu, Mserbia huyo mkongwe alikusanya nguvu upya na kumaliza kazi kwenye seti iliyofuata.

“Nilihisi nimebahatika sana kuokoa ‘break points’ muhimu katika seti ya pili,” Djokovic alisema. “Naamini kwa sehemu kubwa ya seti ya pili na ya tatu, alikuwa mchezaji bora zaidi.”

Djokovic atakutana na Alcaraz kwenye nusu fainali huku Mhispania huyo mwenye umri wa miaka 22 akiwa kwenye kiwango cha juu mno. Bingwa wa mara tano wa Grand Slam alihitaji saa moja na dakika 56 pekee kumshinda kwa urahisi Jiri Lehecka wa Jamhuri ya Czech, anayeshika nafasi ya 20, kwa seti 6-4, 6-2, 6-4.

Alcaraz hajapoteza seti yoyote kwenye safari yake ya kufuzu nusu fainali na mara nyingine tena alikuwa na udhibiti kamili dhidi ya Lehecka.

“Nilicheza mechi nzuri sana — karibu mechi kamilifu,” alisema Alcaraz, ambaye ameshinda mechi 35 kati ya 36 zilizopita tangu kuanza kwa Mashindano ya Italian Open mwezi Mei. “Inaonekana kama, sawa, zimebaki hatua mbili tu, tuone itakuwaje. Lakini naamini najihisi vizuri sana na nina njaa ya kuendelea kushinda.”

  • Sabalenka apita kwa ‘walkover’
    Katika upande wa wanawake siku ya Jumanne, namba moja duniani na bingwa mtetezi Sabalenka alitinga nusu fainali baada ya mpinzani wake wa robo fainali kutoka Jamhuri ya Czech, Marketa Vondrousova, kujiondoa kutokana na majeraha ya goti.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending