Sports
Djokovic Kuzipiga Na Sinner Nusu Fainali Ya Tennis Mjini Wimbledon
Matumani ya bingwa wa mpira wa Tennis Novak Djokovic kupata taji la 25 la Grand slam katika historia ya mchezo huo yangali hai anaposhuka dimbani kwa Nusu fainali dhidi ya mchezaji anayeorodheshwa wa kwanza ulimwenguni kwa sasa Jannik Sinner.
Raia huyo wa Serbia alijitosa kwenye awamu hiyo kwa kushinda Flavio Cobolli raia wa Marekani kwa seti za 6-7 (6/8), 6-2, 7-5, 6-4 katika awamu ya robo fainali mbele ya malkia wa Britain Camila.
Kwa upande wake mchezaji namba moja Jannik Sinner alimpiku mwenzake Ben Shelton raia wa Marekani anayeorodheshwa wa 10 ulimwenguni kwa seti za 7-6 (7/2), 6-4, 6-4.
Katika Nusu fainali ya pili mchezaji anayeorodheshwa wa pili ulimwenguni Carlos Alcaraz kuzipiga dhidi ya Taylor Fritz raia wa marekani.
Upande wa akina dada mwanadada anayeorodheshwa wa kwanza ulimwenguni Aryna Sabalenka atajitosa ugani kucheza dhidi ya Amanda Anisimova raia wa Marekani.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

