Sports
Eliud Kipchoge na bingwa wa Olimpiki Sifan Hassan watasaka ubingwa wao wa kwanza kwenye Marathon ya Jiji la New York mwezi Novemba
Mshikilizi wa zamani wa rekodi ya dunia Eliud Kipchoge na bingwa wa Olimpiki Sifan Hassan watasaka ubingwa wao wa kwanza kwenye Marathon ya Jiji la New York mwezi Novemba, waandaaji New York Road Runners walisema Jumatano.
Wawili hao waliongoza Marathon ya Sydney mwezi uliopita wakati mbio hizo za miaka 25 zikinyanyuliwa hadhi na kuingizwa kwenye mashindano ya World Marathon Majors, na Mholanzi huyo akimaliza kwa muda wa saa 2:18:22.
Hassan, mwanamke wa tatu mwenye kasi zaidi wa muda wote kwenye umbali huo, alimaliza wa tatu London mapema mwaka huu kwa muda wa saa 2:19:00.
Kipchoge mwenye umri wa miaka 40, bingwa wa Olimpiki wa Rio na Tokyo, hajashinda mbio za marathon tangu ushindi wake wa 11 katika majors huko Berlin miaka miwili iliyopita.
Wawili hao wataungana na washiriki wa ngazi ya juu akiwemo mabingwa watetezi Abdi Nageeye wa Uholanzi na Sheila Chepkirui wa Kenya, pamoja na washindi wa zamani Albert Korir na Evans Chebet, wote kutoka Kenya.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

