Sports
Gilbert Lewa Silipwi Ubuntu Fc.
Mkufunzi wa kilabu ya Ubuntu Fc ambaye pia ni mkufunzi wa shule ya Upili ya Majaoni Gilbert Lewa amefichua kwamba halipwi na kilabu yake na kwamba anafanya tu kazi ya kujitolea.
Akizungumza na Kipenga Cha Coco FM mwalimu huyo anasema licha ufanisi ambao wamekua nayo changamoto ni mengi mno kwenye kilabu hiyo.
“Ubuntu silipwi najitolea tu ila ndiyo kilabu imenipa ufanisi na watu kunijua kwa hivyo siwezi nikasema chochote kibaya kwani Ubuntu ni sehemu yangu”.
Hata Hivyo Lewa amesema kwamba Shule Ya Upili Ya Majaoni inamlipa vizuri ndiyo maana akachukua changamoto hiyo mpya akifichua inathiri matokeo ya vijana wake wa Ubuntu Ligi ya Divisheni ya pili kwani hajaenda mazoezini kwa wiki mbili kunoa kilabu yake.
“Majaoni walinitafuta na tukakubaliana na mpaka sasa wananilipa vizuri na tena kwa muda ufao ,Niko na Muda sasa sijaenda kunoa timu ya Ubuntu nilimwachia mwenzangu naambiwa badhi ya wachezaji wanasusia mazoezi kwa sababu mimi ndiyo niliwaleta wanataka kuniona pale uwanjani.”
Ubuntu Fc inaketi nafasi ya sita na alama 33Ligi ya FKF Divisheni ya pili baada ya kutoka sare ya 1-1 na Malindi United.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

