Sports
Gwiji wa Tae-kwon-do Master Kihurani Asherekewa
Gwiji wa mchezo wa tae-kwon-do mwanadada Caroline Wairimu Kihurani ambaye aliaga dunia wiki jana jijini Nairobi anazidi kusherehekewa na wengi kutokana na mchango wake mkubwa katika mchezo huo nchini baada ya kukuza vipaji vingi.
Mchezaji huyo aliingia kwenye daftari za kumbukumbu kwa kuwa mwanamke wa kwanza kuwakilisha Kenya katika mashindano ya dunia ya mchezo huo mwaka 1997 makala ya World Taekwondo Championships mjini Hong Kong Uchina.
Katika ibada ya wafu iliofanyika hapo jana wengi hawakusita kumiminia sifa kedekede mwendazake ambaye aliaga dunia na miaka 57 wakimtaja alikua shujaa kwenye mchezo huo.
Kulingana na Rais wa KTF Major Suleiman Sumba amesema kwamba gwiji huyo hatakumbukwa tu kwa kipaji chake bali pia kwa mchango wake kuwapa msukumo mtoto wa kike.
“Coach Carol kama alivyofahamika hatakumbukwa tu kwa ubora wake uwanjani na kipaji aliyokua nayo kwenye mchezo huu bali pia nyoyo za watoto wengi wa kike ambazo aliwapa nafasi kushiriki mchezo wa tae-kwon-do.
Mwendazake atapumzisha katika makao yake ya milele kule Ol-Joro-Orok siku ya Alhamisi.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

