Sports
Harambee Stars Yavuna Ushindi Dhidi Ya Chad
Timu ya taifa ya soka Harambee Stars imevuna ushindi wa kwanza chini ya kocha Benni McCarthy baada ya kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Chad Ugani Stade De Marrekesh Morocco.
Mshambulizi wa kilabu ya Talanta fc Emmanuel Osoro aliwatanguliza vijana wa nyumbani dakika ya 18 kabila ya mshmabulizi wa Bandari Fc David Sakwa kufunga goli la pili dakika ya 45.
Hata hivyo Chad inayoshikilia nafasi ya 177 kote ulimwenguni ilerejea kwa kishindo kipindi cha pili wakijipatia goli la kufutia machozi dakika ya 60.
Kocha wa Stars anamini angali anajenga kikosi ambacho kitakua bora zaidi katika miaka za mbeleni huku akiahidi vijana wa nyumbani wataleta furaha kwa Wakenya.
“Ushindi ni Muhimu lakini bado najitahidi kuwajua vijana wangu kwa muda mrefu mashabiki wawe na utulivu kwani Stars itafurahisha hivi karibuni.”
Hii ilikua ni ushindi wa kwanza kwa kocha huyo tangu achukuwe mikoba kutoka kwa kocha mkuu Engine Firat alionyeshwa mlango kutokana na msururu wa matokeo duni.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

