Sports
Harambee Stars Yazidi Kujinoa Morocco
Timu ya taifa Harambee Stars imefanya mazoezi ya kwanza nchini Morocco inapojiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Chad hapo kesho.
Vijana wa nyumbani waliwasili nchini humo chini ya kocha Benni McCarthy ambaye ameelezea kwamba kwa sasa anajenga kikosi chenye ubora zaidi kwa siku za usoni
“Ni muda bora mimi kuwajua wachezaji wangu kwani hatujakua pamoja tangu mechi za kufuzu kombe la dunia dhidi ya Gambia na vile vile Gabon,wachezaji niliowaita ni sura ya timu ambayo naiunda si tu kwa Chan bali pia Afcon mwaka 2027 nchini.”
Stars hata hivyo waliwasili bila wachezaji mahiri akiwemo mshambulizi nyota Michael Olunga,kiungo Duke Abuya,Masud Juma,John Ayunga miongoni mwa wnegine kwani bado wako kwenye majukumu ya vilabu vyao ligi za nyumbani.
Timu hiyo inashuka dimbani dhidi ya Chad Juni 6 na Juni 10.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

