Connect with us

Sports

JKA East Africa Gasshuku yazinduliwa Nairobi kwa heshima kubwa

Published

on

Rais wa Chama cha Karate nchini wakili George Kithi amemkaribisha rasmi Shihan Koichiro Okuma, mwalimu kutoka Makao Makuu ya Japan Karate Association (JKA) na Sensei Daniel Gombe kutoka Afrika Kusini, Mkurugenzi wa JKA Kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara, ambao wapo Nairobi kuungana na Sensei Peter Njagi kuongoza mafunzo yaliyosubiriwa kwa hamu ya JKA East Africa Region Gasshuku na Dan Grading. Tukio hili lenye heshima kubwa, lilioandaliwa chini ya mwavuli wa JKA, ni kilele cha kalenda ya sanaa za kijeshi za kikanda na ni fursa muhimu ya kujifunza na kuweka viwango vya juu chini ya wakufunzi wanaotambulika kimataifa.

Tukio hili litafanyika katika Ukumbi wa Mpira wa Kikapu wa Nyayo, eneo lenye uwezo wa kupokea idadi kubwa ya washiriki na watazamaji wanaotarajiwa. Makala ya mwaka huu marufu kama Gasshuku  inawavutia wanakarate kutoka nchi mbalimbali za Kusini mwa Jangwa la Sahara wakiwemo wajumbe kutoka Tanzania, Uganda, Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ethiopia, Togo, Benin, Ghana na Zanzibar. Ushiriki wao unaonyesha ushawishi unaoongezeka na mshikamano wa karate ya JKA katika kanda hii, pamoja na dhamira ya pamoja ya kudumisha viwango vya juu vya nidhamu, mbinu na roho ya mchezo huu.

Katika siku tatu zijazo, kuanzia kesho, washiriki watashiriki katika vipindi vya mafunzo ya kina vitakavyoongozwa na Shihan Okuma na wakufunzi wengine waandamizi. Vipindi hivi vitazingatia kihon, kata na kumite nguzo kuu za Shotokan Karate na kutoa mwanga wa kipekee kuhusu mbinu na falsafa ya karate ya asili. Sehemu ya Dan Grading pia itafanyika wakati huu, ikiwa ni fursa kwa wachezaji waliostahiki kuonyesha ujuzi, uelewa na maendeleo yao chini ya viwango madhubuti vya JKA.

Zaidi ya mafunzo ya kiufundi, Gasshuku ni jukwaa muhimu la kubadilishana tamaduni, kujenga mitandao na kushirikiana kwa kikanda kati ya dojo mbalimbali. Ni wakati si tu wa kuboresha mbinu za karate, bali pia wa kuimarisha dhamira kwa maadili ya heshima, uvumilivu na unyenyekevu yanayoelezea karate-do. Tunatarajia kupata uzoefu wa kipekee, wa kujifunza na usioweza kusahaulika kwa wote watakaoshiriki na kuunga mkono tukio hili.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending