Connect with us

Sports

KCB Rugby Wathibitisha Ubabe kwa Kutwaa Ubingwa wa Kabeberi 7s kwa Ushindi Dhidi ya Daystar Falcons

Published

on

Kilbu ya KCB mchezo wa raga waliendelea kuthibitisha ubabe wao katika National Sevens Circuit baada ya kutwaa taji la Kabeberi 7s kwa ushindi wa alama 20–10 dhidi ya Daystar Falcons kwenye fainali ya Kombe Kuu iliyochezewa uwanjani RFUEA siku ya Jumapili.

Wanabenki hao, ambao sasa wamefungua pengo la alama tisa kileleni mwa msimamo, walionesha ubabe mkubwa katika kipindi cha kwanza kwa kuongoza 20–0 kabla ya kuzima jaribio la vijana wa Falcons waliopambana vikali kipindi cha pili.

Elvis Olukusi aliwapa KCB mwanzo mzuri kwa jaribio la mapema kabla ya Vincent Onyala kuongeza alama baada ya kukamilisha kazi nzuri ya Bob Muhati.

Samuel Asati alifunga jaribio la tatu na kufanya 15–0, kisha Olukusi akaongeza lingine baada ya kunyakua mpira uliokuwa huru, na kuipa KCB uongozi mkubwa hadi mapumziko.

Daystar Falcons walipambana vikali kipindi cha pili na kufunga majaribio mawili, lakini uimara wa ngome ya KCB uliwapa ushindi wa 20–10 na taji la Kabeberi.

Katika nusu fainali, KCB waliwazidi maarifa wapinzani wao Kabras kwa ushindi wa 21–17 katika pambano la kusisimua. Asati na Michael Lukusi walifunga majaribio huku Rayvon Ambale pia akiongeza. Kabras walijibu kupitia Kevin Wekesa na Brian Mutua, lakini jaribio la dakika za mwisho kutoka kwa Floyd Wabwire, lililobadilishwa na Festus Shiasi, liliamua mechi hiyo.

Daystar walitinga fainali baada ya kuwashinda Strathmore Leos kwa alama 12–10. Patrick Odongo alifungua ukurasa wa majaribio kabla ya Clinton Amakuwachi kuongeza la pili. Strathmore walijaribu kurejea kupitia jaribio la Victor Mola, lakini kombora la mabadiliko ya Arnold Mwita lilikosa shabaha.

Kabras walijipatia medali ya shaba baada ya kuwalaza Strathmore Leos 29–12. Mabao mawili ya Kevin Wekesa na jaribio la Brian Mutua yaliwapa uongozi wa 17–0 mapumziko. Licha ya Strathmore kupunguza kupitia Samule Wafula na Victor Mola, jaribio la Mathias Osimbo liliwazima kabisa.

Menengai Oilers waliwafunga Catholic Monks 17–12 kumaliza nafasi ya tano, huku Impala wakiwabugiza Homeboyz 29–0 kwenye fainali ya nafasi ya tisa.

Nakuru waliibuka na ushindi wa 27–5 dhidi ya Embu RFC kutwaa nafasi ya 13, huku Nondescripts wakinyakua taji la Division Two baada ya kuwalaza Zetech Oaks.

Kwa upande wa wanawake, Mwamba waliiburudisha hadhira ya nyumbani kwa kurejea kwa kishindo na kuishangaza Impala kwa ushindi wa 17–12 kupitia sudden death. Impala waliongoza 12–0 mapumziko, lakini Naomi Amugune akawa shujaa kwa Kulabu baada ya kukimbiza mpira kutoka ndani ya eneo lao la 22 na kuvunja ngome ya Impala kufunga golden try.

Ushindi huo umefikisha alama za KCB hadi 104, tisa mbele ya Strathmore Leos. Wanabenki sasa wanahitaji tu kufika nusu fainali ya Kombe Kuu kwenye Dala 7s wiki ijayo ili kutwaa taji la jumla la National Sevens Circuit.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending