Sports
Kikosi cha pili cha Kenya chaelekea Tokyo kwa mashindano ya Riadha Duniani
Kikosi cha pili cha timu ya Kenya kimeondoka nchini Jumatano jioni kuelekea Tokyo, Japan, kushiriki mashindano ya Riadha Duniani kuanzia Jumamosi hii.
Wanariadha waliosafiri kwa kutumia ndege ya Qatar Airways ni pamoja na bingwa wa Olimpiki katika mita 800 Emmanuel Wanyonyi, bingwa wa dunia wa mita 800 kwa chipukizi Sarah Moraa, Nicholas Kebenei, Kelvin Kimtai, Alex Ngéno, Lillian Odira na Vivian Kiprotich, wote wa mita 800.
Wengine ni washiriki wa mbio za mita 5,000, mshindi wa nishani ya shaba mwaka 2023 Jacob Krop, Cornelius Kemboi na Mathew Kipsang.
Makala ya 20 ya mashindano ya Riadha Duniani yataandaliwa kati ya Jumamosi hii Septemba 13 na 21 huku Kenya ikiwakilishwa na wanariadha 58.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

