Connect with us

Sports

Kilabu ya Gor Mahia Iko Tayari Kukabiliana na Simba SC kwenye Simba Day

Published

on

Nahodha wa kilabu ya Gor Mahia, Philemon Otieno, ametangaza kuwa kikosi hicho kiko tayari kwa pambano lao kubwa la maandalizi ya msimu dhidi ya miamba wa Tanzania, Simba SC.

Mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu ya “Simba Day” imepangwa kuchezwa hii leo Jumatano, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, ikianza saa 1:30 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Licha ya mazingira ya kutisha yanayotarajiwa jijini Dar, Otieno ameonyesha kujiamini, akisema kikosi hicho kimejiandaa kikamilifu kwa changamoto hiyo.
“Tuko tayari kwa mechi kubwa, tuko tayari kupambana kwa matokeo chanya,” alisema nahodha huyo.

Miamba hao wa Ligi Kuu ya Kenya waliwasili nchini Tanzania wakiwa na kikosi cha wachezaji 25, huku wakitarajia kuunganishwa na wachezaji watano wa timu ya taifa mara baada ya mechi ya kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Ushelisheli.

Otieno alisifu maandalizi hayo na kusema: “Tumefanya safari vizuri na mapokezi yamekuwa mazuri. Mwaliko huu ni muhimu kwa kuwa Simba ni miongoni mwa timu bora zaidi katika ukanda huu na pia tukizingatia bado tuko katika maandalizi ya msimu mpya, mechi hii ni kipimo kizuri kwetu.”

Pambano hilo linatarajiwa kuwa jaribio muhimu kwa klabu zote mbili ambazo zinakamilisha maandalizi ya vikosi vyao kwa ajili ya misimu ya ndani.

Ingawa historia inatoa matumaini kwa Gor Mahia wakati walipoichapa Simba 2-0 kwenye Super Cup kule Nakuru mwaka 2018 Otieno amesisitiza kuwa malengo yao yapo kwenye mchezo wa sasa.
“Tumecheza na Simba hapo awali lakini yaliyopita si ndwele, tunalenga mechi ya kesho kwa lengo la kupata matokeo bora,” alisisitiza, akipuuza wazo lolote la kutegemea matokeo ya zamani.

Macho yote yatakuwa kwenye namna kikosi cha Gor Mahia, kinachochanganya wachezaji wenye uzoefu na wanaojaribiwa kipindi hiki cha maandalizi, kitakavyokabiliana na presha kali kutoka kwa mashabiki wa nyumbani wa Simba waliopakata uwanja.

Mechi hii inatarajiwa kuwa pambano kali la kusisimua, huku miamba hao wa Kenya wakitafuta kudhihirisha ubabe wao na kujiwekea kasi kuelekea msimu mpya, wakionesha utayari wa kushindana na bora zaidi wa ukanda huu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending