Connect with us

Sports

Kilabu ya KPA Wako Ushindi Mmoja Tu Kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mpira wa Vikapu ya Wanawake

Published

on

Kocha msaidizi wa Kenya Ports Authority (KPA), Samuel Ocholla, ana imani kwamba Wanabandari  hao wataibuka mabingwa wa Ligi ya Mpira wa Vikapu ya Wanawake ya Kenya wikendi hii jijini Nairobi.

Mabingwa hao wa zamani wanaongoza msimamo wa fainali wa mikondo mitano kwa 2-0 baada ya ushindi mfululizo mjini Mombasa, na wakati fainali zikielekea hatua ya uamuzi, ushindi mmoja zaidi dhidi ya Zetech Sparks utatosha kwa KPA kurejesha ubingwa wao wa wanawake.

Watakutana kwa Mchezo wa Tatu Jumamosi katika Ukumbi wa Nyayo kuanzia saa 10 jioni, na iwapo itahitajika, Mchezo wa Nne utafanyika Jumapili katika uwanja huo huo na muda ule ule. Ocholla ameonyesha matumaini kwamba kikosi chake kiko tayari kumaliza kazi licha ya kutarajia upinzani mkali kutoka Zetech Sparks ambao wanataka kugeuza matokeo wakiwa nyumbani.

Timu tayari ipo Nairobi na tunatarajia kushinda, hakuna kingine,” alisema Ocholla kwa kujiamini.

“Tutafanya kazi kwenye maeneo ambayo hatukufanya vizuri Mombasa, huku tukiboresha yale ambayo tulifanya vyema katika michezo ile miwili. Pia tunatarajia mchezo uwe mgumu. Watakuwa wakicheza nyumbani mbele ya mashabiki wao, na watataka kutuletea mchezo. Lakini nia yetu ni kupeleka mchezo kwao.”

Ocholla alisisitiza kwamba kikosi chake kimeazimia kutopoteza nafasi hiyo.

Hatutaruhusu mchezo huo utupite mikononi mwetu. Tunatarajia kumaliza yote, kuchukua ubingwa na kuupeleka tena Mombasa,” aliongeza.

Timu ya KPA imekaribia zaidi kurejesha taji la ligi kuu walilopoteza msimu uliopita kwa Equity Hawks baada ya kupata ushindi mfululizo mjini Mombasa wikendi iliyopita.

Waliibuka na ushindi mwembamba wa 49-48 katika Mchezo wa Kwanza Jumamosi kabla ya kusajili ushindi mwingine mgumu wa 54-49 Jumapili katika Ukumbi wa Makande na kuchukua uongozi wa 2-0 kwenye fainali za mikondo mitano.

Ocholla alisifu uimara na nguvu ya kisaikolojia ya kikosi chake katika michezo hiyo iliyokuwa na ushindani mkali baada ya ushindi huo mara mbili.

“Kwa kuwa ni fainali, tulitarajia michezo mikali sana, na ndivyo hasa tulivyopata,” alisema Ocholla.

Wakiwa na ushindi mbili tayari mfukoni, KPA wanahitaji ushindi mmoja pekee jijini Nairobi ili kutwaa ubingwa na kuthibitisha tena ubabe wao kwenye mpira wa kikapu wa wanawake nchini Kenya.

Mabingwa hao wa zamani sasa wako kifua mbele na watakuwa wakitazamia kufagia mfululizo wote bila kupoteza mchezo wowote watakaporejea dimbani jijini Nairobi, wakilenga kuendeleza ubabe wao katika mpira wa vikapu wa wanawake nchini.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending