Connect with us

Sports

Kocha John Baraza Atemwa na Bandari baada ya Ujio wa Kocha Mpya Borji

Published

on

Kocha mkongwe John Baraza ameagana rasmi na klabu ya Bandari FC, siku mbili tu baada ya klabu hiyo kumtambulisha Mohammed Borji kama kocha mkuu mpya, huku Tarik Bendamou akiteuliwa kuwa kocha msaidizi.

Kulingana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Bandari FC, Tony Kibwana, uamuzi wa kumaliza muda wa Baraza ulifikiwa kwa makubaliano ya pande zote mbili. Mkataba wa Baraza wa miaka miwili, ambao ulipaswa kukamilika Januari 2026, ulisitishwa baada ya mazungumzo baina ya pande hizo mbili.

“Baada ya ujio wa kocha mpya, tulikutana na Kocha Baraza kumueleza mipango yetu. Kwa bahati mbaya, hakukubaliana nayo,” alisema Kibwana.
“Tukakubaliana kuachana, miezi mitatu kabla ya mkataba wake kuisha. Ameitumikia klabu vizuri, na tunamtakia kila la heri katika safari yake ya baadaye.”

Kocha huyo wa zamani wa Mara Sugar na Kakamega Homeboyz alijiunga na Bandari FC mnamo Oktoba 2023 kufuatia kufutwa kazi kwa kocha mkongwe Twahir Muhidin.

Alithibitishwa kama kocha mkuu Januari 2024 na kusaini mkataba wa miaka miwili hadi 2026.

Wakati wa uongozi wake, Baraza alibadilisha mwenendo wa timu — akiipandisha Bandari kutoka nafasi ya 11 hadi nafasi ya 4 katika msimu wa Ligi Kuu ya Kenya (KPL) wa 2023–2024.

Hata hivyo, jukumu lake lilibadilika Julai 2024 aliposhushwa cheo kuwa kocha msaidizi, huku Ken Odhiambo, aliyewahi kuwa kocha msaidizi wa Harambee Stars, akichukua nafasi ya kocha mkuu.

Chini ya uongozi huo mpya wa kiufundi, Bandari FC ilimaliza msimu wa 2024–2025 katika nafasi ya 8, ikikusanya alama 44 kutokana na ushindi 10, sare 14, na vipigo 10.

CEO Kibwana alionyesha matumaini licha ya changamoto za hivi karibuni na akatoa wito kwa mashabiki kuunga mkono benchi jipya la ufundi.

“Kocha wetu mpya, Borji, na msaidizi wake wanaelewana vizuri na wachezaji,” alisema.
“Wachezaji wamepokea vyema mbinu mpya za mazoezi na mitindo ya mchezo, na tunaamini matokeo mazuri yatakuja hivi karibuni.”

“Tunawaomba mashabiki wawe na subira tunapoendelea kujenga timu imara kwa ajili ya KPL,” aliongeza Kibwana.

Bandari FC inatarajiwa kukutana na AFC Leopards kesho katika Uwanja wa Mbaraki kwenye mashindano ya ODM @20, ambayo yanashirikisha timu kubwa kama Gor Mahia na Shabana FC.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending