Connect with us

Sports

Kocha wa Bandari FC Ken Odhiambo: Tupo Tayari Kumaliza Kazi Dhidi ya Shabana

Published

on

Kocha mkuu wa Bandari FC, Ken Odhiambo, ameonyesha kujiamini kuwa kikosi chake kipo tayari kurejea kwenye njia ya ushindi, wanapowakaribisha Shabana FC Jumapili alasiri kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Kenya (KPL) itakayochezewa Uwanja wa Mbaraki, Mombasa.

Bandari walishikiliwa kwa sare tasa na Kariobangi Sharks katika mchezo wao wa kwanza wa msimu, lakini Odhiambo anaamini kikosi chake kimejifunza kutokana na makosa hayo na kiko tayari kujibu vyema nyumbani.

“Tulikuwa na bahati mbaya tu katika mechi ya ufunguzi,” alisema kocha huyo. “Lakini tumejifunza na tupo tayari kurekebisha mambo dhidi ya Shabana. Hapa Mbaraki, lengo letu ni alama zote tatu — na lazima tuanze na mechi dhidi ya Shabana, japo tunajua haitakuwa rahisi.”

Hata hivyo, Bandari wanakumbwa na changamoto za majeruhi, huku wachezaji muhimu Dennis Ng’ang’a, Swaleh Pamba, na mshambuliaji Beja Nyamawi wakiwa bado hawajapona. Ng’ang’a alipata jeraha kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Yanga SC ya Tanzania, Pamba akiwa na hali ya usawa wa 50%, huku Beja akiumwa na goti lililovimba.

“Nina matumaini kuwa kufikia Ijumaa baada ya tathmini, huenda wakawa tayari kwa uteuzi,” aliongeza Odhiambo.

Kocha huyo pia ametoa wito kwa mashabiki wa Bandari kujitokeza kwa wingi kuipa nguvu timu Jumapili hii, akisisitiza mchango mkubwa wanaocheza kama “mchezaji wa 12”.

“Tunapaswa kutumia mechi yetu dhidi ya Yanga kama mfano wa kile mashabiki wanaweza kufanya wakati wa mchezo. Mashabiki ni wachezaji wa 12 — wanabeba nafasi kubwa kwa timu yoyote yenye mafanikio. Tunawaomba waje kwa wingi kutusukuma Jumapili dhidi ya Shabana,” alisema Odhiambo.

Mechi hiyo inatarajiwa kuanza saa tisa alasiri (3:00 PM) katika Uwanja wa Mbaraki, huku Bandari wakilenga ushindi wao wa kwanza wa msimu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending