Connect with us

Sports

Kocha wa Stars Benni Mccarthy Ana Imani Kupata Ushindi dhidi ya Madagascar Robo Fainali CHAN Kasarani

Published

on

Kocha mkuu wa Harambee Stars, Benni McCarthy, ameonyesha imani kubwa huku kikosi chake kikijiandaa kwa pambano la kihistoria la robo fainali dhidi ya Madagascar litakalochezwa katika Uwanja wa Kimataifa wa Moi, Kasarani, Ijumaa, Agosti 22 saa 11 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari kabla ya mechi akiwa ameandamana na nahodha msaidizi Daniel Sakari, McCarthy amesema safari ya Stars katika hatua ya makundi imewaimarisha kwa hatua ya muondoano.

Kenya iliongoza katika kundi gumu lililojumuisha DR Congo, Angola, Morocco na Zambia na kufanikisha tiketi ya kufika robo fainali.
“Baada ya mtihani tulioupitia hatua ya makundi, nafikiri hakuna timu ambayo tunaogopa tena. Fursa zetu zilikuwa finyu, lakini tulijithibitisha kwamba tuna uwezo wa kuvuka vikwazo hivyo. Yeyote atakayekuja mbele yetu atakuwa changamoto nzuri, lakini mtazamo wetu ni sisi wenyewe na kusonga hatua inayofuata,” alisema McCarthy.

Mtaalamu huyo kutoka Afrika Kusini alibainisha maandalizi yake yanahusisha zaidi ya mbinu, akisisitiza uimara wa kisaikolojia.

“Nafanya kazi ya kujenga utulivu wa kiakili ndani ya wachezaji wangu. Matumaini yako juu, lakini tulifanya uchambuzi wetu wa wapinzani watarajiwa. Madagascar watakuwa kizuizi kingine, na haijalishi tulichokipata kabla, kimesahaulika. Tunapaswa kujiandaa kadiri tuwezavyo,” alisisitiza McCarthy.

McCarthy alithibitisha kuwa hakuna majeraha makubwa kuelekea robo fainali. Mchezaji pekee atakayekosa ni Chrispine Erambo, aliyesimamishwa baada ya kadi nyekundu wakati wa ushindi wa Stars wa 1-0 dhidi ya Morocco.

Akitambua ubora wa kipa Byrne Omondi aliyeibuka shujaa wa mechi, McCarthy aliwataka wachezaji wake kuongeza makali ya safu ya ushambuliaji.

Ushindi dhidi ya Madagascar utaipeleka Kenya kwenye nusu fainali dhidi ya mshindi kati ya Algeria na Sudan watakaovaana Jumamosi, Agosti 23, kule Zanzibar.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending