Sports
Kocha Wa Stars Mccarthy Ataja Kikosi Cha Mwisho Kombe La CHAN
Mkufunzi wa timu ya soka Harambee Stars Benni Mccarthy amekitaja kikosi chake cha mwisho chenye wachezaji 25 tayari kwa kombe la Chan mwezi ujao,vijana wa nyumbani wakifungua dimba dhidi ya DR.Congo Agosti 3 ugani Kasarani.
Miongoni mwa nyota waliojumuishwa kikosini ni pamoja na kipa mzoefu wa kilabu ya Bandari FC Faruk Shikhalo,beki wa Police Aboud Omar ambaye atakua nahodha wa kikosi hicho pamoja na viungo Austine Odhiambo,Marvin Nabwire na mshambulizi Masoud Juma ataongoza safu ya mashambulizi pamoja na Ryan Ogam wa kilabu ya Tusker Fc.
Magolikipa;
Faruk Shikhalo, Byrne Omondi, Sebastian Wekesa
Mabeki;
Siraj Mohammed, Manzur Suleiman, Pamba Swaleh, Abud Omar, Alphonce Omija, Sylvester Owino, Mike Kibwage, Daniel Sakari, Lewis Bandi, Kevin Okumu
Viungo;
Brian Musa, Alpha Onyango, Austin Odhiambo, Ben Stanley, Marvin Nabwire
Washambulizi;
Mohammed Bajaber, Boniface Muchiri, David Sakwa, Ryan Ogam, Masoud Juma, Austin Odongo, Felix Oluoch
Stars wako kundi A pamoja na Angola,DR.Congo,Morocco na Zambia.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

