Connect with us

Sports

Liverpool Kupata Mtihani Mkubwa Dhidi ya Crystal Palace Ligi ya Epl Wikendi hii

Published

on

Kilabu ya Liverpool, ambao hawajapoteza mechi yoyote katika utetezi wao wa taji la Ligi Kuu msimu huu, wanakabiliwa na mtihani kubwa watakapokutana na Crystal Palace ambao pia hawajafungwa, Jumamosi.

Palace tishio kwa Liverpool
Liverpool wameanza msimu kwa kishindo kwa kushinda mechi saba mfululizo katika mashindano yote. Wakiwa kileleni mwa jedwali, wamejikusanyia alama tano zaidi ya wapinzani wao baada ya ushindi mara tano mfululizo kwenye ligi.

Hata hivyo, kikosi cha Oliver Glasner (Palace) kipo kwenye kiwango kizuri pia, kikiwa nafasi ya tano. Wao ndio mabingwa wa Kombe la FA na timu pekee nyingine isiyoshindwa kwenye ligi kuu. Palace tayari wameshaonja mafanikio dhidi ya vijana wa Arne Slot, wakiwafunga kwa penalti kwenye mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) Wembley mwezi Agosti.

Msimu uliopita, Palace walitoka sare ya 1-1 na Liverpool katika uwanja wa Anfield kwenye siku ya mwisho ya ligi, matokeo yaliyokuwa sehemu ya rekodi yao ya kutofungwa mechi 16 mfululizo tangu Aprili.

Kwa kutokuwepo kwa Hugo Ekitike (aliyesimamishwa), usajili wa rekodi ya Uingereza Alexander Isak anatarajiwa kuongoza safu ya ushambuliaji ya Liverpool, baada ya kufunga bao lake la kwanza katikati ya wiki dhidi ya Southampton kwenye Kombe la Ligi.
Atakabiliwa na changamoto kutoka kwa Marc Guehi, beki wa timu ya taifa ya England wa Palace, ambaye alikaribia kujiunga na Liverpool kabla ya uhamisho kuvunjika siku ya mwisho ya dirisha la usajili.


Hakuna nafasi ya makosa kwa Arsenal
Arsenal, wanaotafuta taji lao la kwanza la ligi tangu 2004, hawawezi kumudu kupoteza tena wanapokabiliana na Newcastle Jumapili.

Kikosi cha Mikel Arteta, kilichomaliza nafasi ya pili mara tatu mfululizo, tayari kimeachwa nyuma ya Liverpool baada ya kupoteza dhidi ya mabingwa Anfield na kutoa sare na Manchester City.

Arsenal pia wamefungwa katika safari zao tatu zilizopita St James’ Park, ikiwemo kichapo kwenye nusu fainali ya Kombe la Ligi msimu uliopita. Newcastle, ambao wameshinda mechi nne kati ya sita za mwisho dhidi ya Arsenal, wana hamasa kubwa baada ya kupata pointi sita pekee katika mechi zao tano za kwanza.


Amorim atafuta mwendelezo na Man United
Kocha wa Manchester United Ruben Amorim anatarajia kupata ushindi wa pili mfululizo wa ligi timu yake ikipambana na Brentford Jumamosi.

Tangu afike kutoka Sporting Lisbon mwezi Novemba, Amorim amekumbana na changamoto kubwa ikiwemo kufungwa na timu ya daraja la nne Grimsby kwenye Kombe la Ligi mwezi Agosti. Hata hivyo, United wamepata afueni kwa ushindi wa nyumbani dhidi ya Burnley na Chelsea — mara ya kwanza chini ya Amorim.

Lakini bado presha ipo baada ya kupoteza vibaya 3-0 dhidi ya Manchester City, matokeo yaliyofichua udhaifu mkubwa wa kikosi chake.

Iwapo United hawatarejea na pointi tatu kutoka Brentford, ambao wako nafasi ya 17 baada ya kupoteza mechi tatu kati ya tano chini ya Keith Andrews, presha kwa Amorim itaongezeka zaidi.


Ratiba ya Mechi za EPL
Jumamosi

  • Brentford v Manchester United (2.30pm)

  • Chelsea v Brighton 5.00pm

  • Crystal Palace v Liverpool

  • Leeds v Bournemouth

  • Manchester City v Burnley

  • Nottingham Forest v Sunderland (7.30pm)

  • Tottenham v Wolves (10.00pm)

Jumapili

  • Aston Villa v Fulham (4.00pm)

  • Newcastle v Arsenal (6.30pm)

Jumatatu

  • Everton v West Ham (10.00pm)

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending