Sports
Lyon Yashushwa Ngazi Ligi One Ya Ufaransa
Kilabu ya Olimpiki Lyon Ya Ufaransa imeshushwa ngazi katika ligi hiyo Ligi 1 hadi ligi ya daraja ya pili marufu kama Ligi 2 na chama cha soka cha uchunguzi Ufaransa kwa ubadirifu wa fedha.
Duru za kuaminika zasema kwamba mabingwa hao mara saba wa ligi one wamekua wakitumia hela nyingi kuwasajili wachezaji bila kupata faida yoyote au akaunti zao kupokea hela zozote kwa misimu 2.
Hata hivyo mmiliki wa kilabu hiyo John Texter amesema kwmaba wana imani uamuzi huo utabatilisha kwani wanakwenda kukataa rufaa dhidi ya uwamuzi huo kwa kilabu hiyo.
Lyon walimaliza nafasi ya sita jedwali la ligi ya Ufaransa na walikua kwenye kombe Europa ila huenda hilo likatatiza mipango yao ya msimu ujao.
Kilabu hiyo haijacheza katika ligi daraja ya pili tangu mwaka 1987 na walikua wamepngia kwamba kambi ya mazoezi Julai 7.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

