Sports
Mabondia Wawili Wafariki Nchini Japan Baada ya Mapigano Tofauti
Mabondia wawili nchini Japan wamefariki dunia baada ya kupata majeraha makubwa katika mapigano mawili tofauti yaliyofanyika jijini Tokyo wikendi hii.
Bondia wa uzani wa Super Featherweight, Shigetoshi Kotari, na mwenzake Hiromasa Urakawa, wote wakiwa na umri wa miaka 28, walikimbizwa hospitalini baada ya kupoteza fahamu katika mapigano yao tofauti.
Wanabondia hao walihitaji kufanyiwa upasuaji wa ubongo, lakini hata hivyo walipoteza maisha wakiwa hospitalini.
Kotari alipoteza fahamu wakati wa pambano lake dhidi ya Yamato Hata, na licha ya juhudi za madaktari baada ya kukimbizwa hospitalini, alifariki saa nne usiku.
Urakawa naye alipoteza fahamu katika raundi ya nane ya pambano lake dhidi ya Yoji Saito. Pigano hilo lilikatishwa na alihamishiwa hospitalini, ambako alifariki usiku wa Jumamosi.
Chama cha Mabondia nchini Japan kilitoa salamu za rambirambi, na kupitia kwa Mkurugenzi wake Mtendaji Tsuyoshi Yasukochi, kilieleza masikitiko makubwa, kikisema kuwa hii ni mara ya kwanza katika historia ya mchezo huo nchini humo kwa mabondia wawili kupoteza maisha ndani ya kipindi kimoja.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

