Sports
Madereva Wa KCB Kukabana Koo Rwanda Mountain Gorilla Rally
Madereva zaidi ya 35 kuzindua uhasama katika makala ya mwaka huu ya Rwanda Mountain Gorilla Rally ikiwa ni raundi ya taji la Bara Afrika Julai 4 hadi Julai 6 mjini Kigali Rwanda.
Dereva wa Kenya Karan Patel amesema kwamba anatarajia upinzani mkubwa kutoka kwa Yasin Nasser raia wa Uganda ambaye amejinyakulia pointi 63 na ndiye anaongoza chati mashindano ya magari Barani Afrika,African Rally Championship.
Madereva wengine ambao wako kwenye kinyanganyiro cha kusaka taji hilo ni pamoja na Nikhil Sachania na Carl Flash Tundo ambao wote wanashika nafasi ya pili na alama 50.
Tineja Jeremiah Wahome ameketi nafasi ya nne na pointi 42 akifuatwa na Samman Vohra naye Karan Patel akiketi nafasi ya sita na pointi 35.
Madereva wengine watakaoshiriki ni Michael Muluka wa Uganda na Queen Kalimpinya wa Rwanda.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

