Connect with us

Sports

Mashabiki wa Arsenal kutoka Kenya wamtunuku heshima marehemu Raila Odinga kwa ziara ya kihistoria Bondo

Published

on

Mamia ya mashabiki wa Klabu ya Soka ya Arsenal kutoka matawi manane nchini Kenya walitembelea Kang’o Kajaramogi katika Eneo Bunge la Bondo kuonyesha heshima zao kwa marehemu Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga, ambaye alikuwa shabiki sugu wa timu hiyo ya Ligi Kuu ya Uingereza.

Wakiongozwa na Silas Odhiambo, mashabiki hao waliovaa jezi nyekundu na nyeupe zinazotambulisha klabu hiyo, waliwasili mapema asubuhi na kuelekea moja kwa moja kwenye kaburi la Odinga.

Hapo walitumbuiza wimbo wa North London Forever, wimbo rasmi wa Arsenal, kama ishara ya heshima ya kihisia kwa mmoja wa mashabiki wenzao.
Akizungumza baada ya ibada fupi ya maombi, Odhiambo alisema ziara hiyo ilikuwa ni ishara ya heshima kwa upendo wa dhati aliokuwa nao Odinga kwa klabu hiyo.

“Marehemu Odinga alikuwa shabiki wa kweli wa Arsenal, na sisi kama mashabiki wenzake tumejitokeza kusherehekea mapenzi yake kwa timu na maadili aliyoyawakilisha,” alisema.

Kikundi hicho baadaye kilitembelea nyumbani kwa familia ya Odinga katika Shamba la Opoda, ambapo Mama Ida Odinga na Raila Odinga Junior waliwapokea kwa moyo mkunjufu.

Familia ya Odinga ilitoa shukrani za dhati kwa mashabiki hao kwa ziara yao, ikibainisha jinsi marehemu Odinga alivyoithamini sana uhusiano wake na Arsenal na jumuiya yake ya kimataifa.

Raila Odinga, ambaye alizikwa Jumapili iliyopita, alijulikana sana kwa uaminifu wake usiokuwa na kifani kwa Arsenal — mapenzi yaliyomfanya apendwe na mashabiki wengi wa soka kote nchini.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting

Published

on

By

Mshambuliaji Kai Havertz aliifungia Arsenal F.C. bao la ushindi katika dakika za mwisho kabisa, na kuisaidia timu hiyo kuibuka na ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Sporting CP katika mechi ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya UEFA Champions League iliyochezwa Jana usiku.

Kikosi cha kocha Mikel Arteta kilifika katika Uwanja wa Estadio Jose Alvalade kikiwa kimeathiriwa na vipigo viwili mfululizo dhidi ya Manchester City F.C. kwenye fainali ya Kombe la Ligi na Southampton F.C. katika robo fainali ya Kombe la FA.

Kwa mara nyingine, Arsenal haikucheza kwa kiwango chake bora, lakini ilifanikiwa kupata ushindi kutokana na uokoaji mzuri wa kipa David Raya pamoja na umakini wa Havertz aliyefunga bao la ushindi katika muda wa nyongeza.

Arsenal sasa ina nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali kabla ya mechi ya marudiano itakayochezwa kaskazini mwa London tarehe 15 Aprili, ingawa italazimika kuboresha kiwango chake ikiwa inataka kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza.

Vipigo dhidi ya City na Southampton vilikuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Arsenal kupoteza mechi mbili mfululizo, huku kipigo cha Kombe la FA kikiwa cha tano kwao msimu huu.

Athari za matokeo hayo bado zilionekana Lisbon, ambapo Arsenal ilipata ugumu wa kucheza kwa mwendelezo mzuri, lakini kama ilivyokuwa mara kadhaa msimu huu, walipata njia ya kushinda licha ya kutocheza vizuri.

katika mechi nyingine hatua ya robo fainali ni kwamba Bayern Munich waliondoka na ushindi wa magoli 2-1 mikononi mwa Real Madrid katika uwanja wao wa nyumbani Estadio Santiago Bernabeu.

Magoli ya Bayern yakitiwa kimyani na mshmabulizi Luis kipindi cha kwanza naye Erling Haaland kipindi cha pili.

Mechi ya marudiano itachezwa juma lijalo April 15.

Continue Reading

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Trending