Sports
Mashindano Ya Dunia Ya Handiboli Ya Ufukweni Kuanza Rasmi Tunisia
Kikosi cha Taifa mchezo wa Handiboli wachezaji chipukizi kuanza rasmi mashindano ya kombe la dunia hapo kesho mjini Tunis Tunisia.
Kulingana na droo iliyofanywa hii leo ni kwamba timu zote mbili upande wa wanaume na akina dada zimejumuishwa kundi B huku kikosi cha akina dada ikiratibiwa kumenyana na mataifa ya Uholanzi,Ujerumani,Rep of China kunid A zina timu za Ufaransa,Brazil,Thailand na Tanzania.
Kundi C zina timu za Tunisia,Hungary,Mexico na Senegal, Kundi la mwisho kundi D zina timu za Croatia,Uruaguay,Uhispania na Bulgaria.
Upande wa wanaume Kenya itamenyana na Hungary,Ujerumani na Tanzania huku kundi A likiwa na timu za Iran,Uhispania,Oman na Puerto Rico,Kundi C linajumuisha timu za Tunisia,Thailand,Mexico na Cook Island huku kundi D likiwa na timu Argetina,Brazil,Uruguay na Senegal.
Mashindano hayo yanaanza kesho na kukamilika Juni 22.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.


Titus Kesekwa
June 16, 2025 at 4:55 pm
Kazi safi sana kaka na Coco tv/radio.