Sports
Mbeumo United Ndiyo Chaguo Langu
Kiungo mshamabulizi wa kilabu ya Brenford na Cameroon Bryan Mbeumo ameweka wazi kuwa anapendelea kujiunga na kilabu ya Manchester United pekee msimu huu.
Mchezaji huyo ambaye alifunga magoli 20 msimu uliopita anasema hatakubali ofa kwiengineko iwapo united hawataendelea na dili hio kumpeleka Old Trafford.
Kilabu ya Manchester United wanatarajiwa kuwasilisha ofa ya pili kusaka hudumza za winga huyo,
Hii ni baada ya ofa ya kwanza ya pauni milioni 55 kukataliwa na Brenford wiki moja iliopita.
Brenford wanataka pauni milioni 60 kumwachilia mchezaji huyo nyota ambaye pia anamezewa mate na kilabu ya Tottenham Ya Uingereza.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

