Connect with us

Sports

Mchezaji tineja David Nyangige Ajumuishwa kwa Kikosi cha Shujaa kinachojiandaa HSBC SVNS Nyayo

Published

on

Mchezaji kikosi cha Morans David Nyangige ni miongoni mwa wachezaji walioshtua wengi baada ya kujumuishwa katika kikosi cha Shujaa kilichotangazwa Jumatatu na kocha Kevin ‘Bling’ Wambua, wakati timu hiyo ikijiandaa kwa mashindano ya HSBC SVNS yatakayofanyika mwishoni mwa wiki hii katika Uwanja wa Nyayo.

Kikosi hicho cha wachezaji 12 kitaongozwa na nahodha George Ooro huku Samuel Asati akihudumu kama nahodha msaidizi. Wengine waliotajwa ni John Okoth, Dennis Abukuse, mkongwe Vincent Onyala, Kevin Wekesa, Patrick Odongo, Festus Shiasi, Nygel Amaitsa, Floyd Wabwire na Chrisant Ojwang.

Kocha Wambua alionyesha imani kubwa kwa kikosi chake akibainisha kuwa mashabiki wa nyumbani watatoa hamasa ya kipekee, hasa baada ya tiketi zote kuuzwa.

“Shinikizo tutakalopata tunalipokea kwa mikono miwili. Tukiwa nje ya nchi hupata nguvu kutoka kwa kona ya Wakenya, lakini wiki hii uwanja mzima ni kona ya Kenya. Tuna imani hilo litatupa msukumo mkubwa,” alisema Wambua.

Nahodha msaidizi Samuel Asati pia alieleza furaha yake kucheza nyumbani.

“Ni heshima kubwa kwangu kucheza nyumbani mwishoni mwa wiki hii. Tutafanya kila tuwezalo kuiletea nchi fahari tunapowania kufuzu kwa Divisheni ya Kwanza,” alisema Asati.

Kwa upande wa timu ya wanawake, Lionesses, kocha Simon Odongo amewajumuisha kwa mara ya kwanza Marvel Oswago na Charity Nilah. Wataungana na Naomi Amumgumi, Maureen Muritu, Sheila Chajira (Nahodha), Sinaida Nyacho, Edith Nariaka, Janet Okello, Freshia Oduor (Nahodha Msaidizi), Grace Okulu, Stella Wafula na Phoebe Akinyi.

Odongo alisifu uzoefu wa wachezaji wake wa kimataifa akisema unaongeza nguvu kikosini.

“Tunalenga kuipeperusha bendera ya Kenya juu wikendi hii mbele ya mashabiki wetu wa nyumbani,” alisema Odongo.

Katika mechi za ufunguzi, Shujaa watamenyana na Canada, Ubelgiji, Ujerumani, Uruguay na Marekani, huku Lionesses wakikabiliana na Brazil, China, Afrika Kusini, Argentina na Hispania.

Mashindano hayo yataanza Februari 14, yakifungua rasmi kampeni ya timu zote mbili ya kusaka nafasi ya kupanda Divisheni ya Kwanza. Kwa sasa Kenya ipo Divisheni ya Pili, lakini kumaliza miongoni mwa timu nne bora katika mfululizo wa mashindano ya raundi tatu kutawapa nafasi ya kupanda daraja, huku raundi ya kwanza ikifanyika nyumbani.

Wakati huo huo, mpango wa kukuza vipaji vya vijana wa Shirikisho la Raga Kenya umepata msukumo baada ya Kampuni ya Kenya Power (KPLC) kuahidi kutoa shilingi milioni 3 kusaidia programu za maendeleo ya raga mashinani. Wawakilishi wa KPLC walisisitiza umuhimu wa kulea vipaji vya vijana ili kuimarisha mustakabali wa raga nchini.

Hii hapa ni kikosi kamili cha Shujaa;

Shujaa:

George Ooro(Captain)

Samuel Asati (Co Captain)

John Okoth

Dennis Abukuse

Vincent Onyala

Kevin Wekesa

Patrick Odongo

Festus Shiasi

Nygel Amaitsa

Floyd Wabwire

Chrisant Ojwang

David Nyangige (Debut)

Lionesses

Naomi Amumgumi

Moreen Muritu

Sheila Chajira(Captain)

Sinaida Nyacho

Edith Nariaka

Janet Okello

Marvel Oswago (Debut)

Freshia Oduor (Co captain)

Charity Nilah (Debut)

Grace Okulu

 Stella Wafula

Phoebe Akinyi

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)

Published

on

By

Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.

Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.

SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

Continue Reading

Sports

Bingwa wa dunia mbio za mitaa 1500 Faith Kipyegon ateuliwa kuwania tuzo za kila mwaka za ‘Laureus World Sportswoman of the Year.’

Published

on

By

Nyota wa mbio za masafa ya kati kutoka Kenya, Faith Kipyegon, amepata uteuzi wake wa tatu mfululizo kuwania tuzo ya Mwanamichezo Bora wa Kike wa Mwaka katika hafla maarufu ya Laureus World Sports Awards, hatua inayozidi kuthibitisha ubabe wake katika kizazi hiki cha wanariadha.

Tuzo hizo, zinazotambuliwa kimataifa kama “Oscars za Michezo”, huandaliwa na Laureus Sport for Good Foundation na hulenga kutambua mafanikio ya kipekee, uthabiti na mchango chanya wa michezo duniani.

Uteuzi wa Kipyegon kwa miaka mitatu mfululizo unaonyesha si tu kipaji chake, bali pia uimara wa kiwango chake cha juu kwa muda mrefu. Mwaka 2024 aliteuliwa baada ya msimu wa kihistoria wa 2023 ambapo alivunja rekodi tatu za dunia na kushinda dhahabu mbili katika Mashindano ya Dunia.

Mwaka 2025 alirejea tena kwenye orodha ya wateule kufuatia mafanikio makubwa katika Michezo ya Olimpiki ya Paris, ambako aliweka historia kwa kuwa mwanamke wa kwanza kushinda medali tatu za dhahabu mfululizo katika mbio za mita 1,500.

Sasa mwaka 2026, anawania tuzo hiyo tena baada ya kuvunja rekodi yake mwenyewe ya dunia ya mita 1,500 na kutwaa taji lake la nne la dunia katika msimu bora wa 2025.

Katika kinyang’anyiro cha mwaka huu, Kipyegon anakutana na ushindani mkali kutoka kwa nyota wengine wa kimataifa akiwemo Sydney McLaughlin-Levrone, Melissa Jefferson-Wooden, Aitana Bonmati, Aryna Sabalenka, na Katie Ledecky.

Uteuzi huu unaendeleza hadhi ya Kipyegon kama mmoja wa wanariadha bora zaidi duniani na fahari kubwa kwa Kenya katika jukwaa la kimataifa.

Continue Reading

Trending