Sports
Mshambulizi wa Leicester Jamie Vardy ajiunga na Cremonese ya Serie A
Mshambulizi wa Uingereza Jamie Vardy, ambaye mabao yake yaliipeleka Leicester City kutwaa taji la kipekee la Ligi Kuu ya England mwaka 2016, amejiunga na kikosi kipya kilichopanda ligi ya Serie A, Cremonese, siku ya Jumatatu.
Vardy mwenye umri wa miaka 38, ambaye alikuwa mchezaji huru tangu aondoke Leicester mwezi Mei, amesaini mkataba wa mwaka mmoja ukiwa na chaguo la kuongezwa, saa chache kabla ya dirisha la usajili kufungwa, klabu hiyo ya Italia imetangaza.
Mchezaji huyo aliyefunga mabao 145 ya Ligi Kuu ya England katika mechi 342, anaingia kwenye timu ambayo imeshinda mechi zake mbili za mwanzo za Serie A, ikiwemo ushindi wa 2-1 dhidi ya AC Milan katika uwanja wa San Siro.
Vardy anajiunga na kundi linalokua la wachezaji wa zamani wa Ligi Kuu ya England walioko Serie A.
Miongoni mwao ni Scott McTominay, ambaye amepata mafanikio tangu kuondoka Manchester United na kujiunga na Napoli, akiisaidia timu hiyo ya kusini mwa Italia kutwaa ubingwa wa Serie A mwezi Mei.
Msimu huu ameunganishwa Napoli na Kevin De Bruyne, nyota wa zamani wa Manchester City.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

